TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Thursday, October 8, 2009

Haki itendeke asema Kofi Annan

8:18 AM

Aliyekuwa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan amesema waliyoongoza ghasia zilizoibuka baada ya uchaguzi mkuu nchini Kenya lazima wafikishwe mahakamani.

Wahusika wakuu wa vurugu hizo watafikishwa katika mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita huko Hague, ICC.

Hata hivyo, Bw Annan amesema ni muhimu wengine wahukumiwe Kenya.

Bw Annan alisaidia katika upatanishi wa kuleta amani baada ya ghasia za mwaka 2008 ambapo watu 1,300 waliuawa na 300,000 walihama makazi yao.

Pia ameonya kuwa Kenya inahitaji kuharakiza mabadiliko iwapo wanataka kuepusha ghasia nyingine kuibuka tena.

Katika siku ya mwisho ya ziara yake ya siku tatu nchini Kenya, Bw Annan amesema serikali imemhakikishia kuwa itashirikiana na mahakama ya ICC.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA