TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Saturday, September 26, 2009

Maharamia washambulia meli Mogadishu

8:17 AM

Maharamia kutoka Somalia wamepanda meli iliyokuwa ikielekea katika bandari ya Mogadishu na kumwuua kwa kumpiga risasi nahodha wa chombo hicho ambaye ni raia wa Syria.

Maafisa wamesema nahodha wa meli hiyo alikataa kutii matakwa ya maharamia hao iliyomtaka asielekee kwenye bandari hiyo.

Inaaminiwa hili ni shambulio la kwanza la aina yake kutokea karibu na mji mkuu wa Somalia.

Maharamia wana desturi ya kufanya mashambulio yao maeneo ya kaskazini, hasa karibu na Eyl.

Askari wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika na majeshi ya usalama ya Somalia walivamia na kuweza kuokoa meli hiyo yenye bendera ya Panama.

Hata hivyo, mabaharia watatu nao wameripotiwa kujeruhiwa katika shambulio hilo.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA