
Waziri wa Mambo ya Kigeni wa Marekani Bi Hillary Clinton amewasili nchini Nigeira akiwa katika hatua yake ya tano ya ziara ya kutembelea mataifa saba ya bara la Afrika.
Wakati wa ziara yake hiyo ya saa 36 Bi Clinton atakutana na waziri mwenzake wa Mambo ya nje wa Nigeria, Ojo Maduekwe na baadae atafanya mazungumzo na Rais Umaru Yar'Adua.
Wachambuzi wa mambo wanasema waziri huyo wa Marekani atakuwa mkali katika suala zima la rushwa na mageuzi yanayosimamia uchaguzi.
Mwezi uliopita Rais wa Marekani Barack Obama aliiruka Nigeria wakati wa ziara yake ya kwanza rasmi barani Afrika kutokana na kile kilichoonekana rekodi mbovu ya utawala bora.
0 comments:
Post a Comment