TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Tuesday, June 30, 2009

Mawaziri wa MDC wamsusia Mugabe

11:53 AM
http://www.huffingtonpost.com/huff-wires/20090211/af-zimbabwe/images/8f2a9159-2890-4927-b226-77232bb7fdfa.jpg
Mawaziri kutoka chama cha Movement for Democratic Change (MDC) nchini Zimbabwe wamesusia kikao cha baraza hilo kilichoendeshwa chini ya uenyekiti wa rais Robert Mugabe.

Mkutano huo, ambao hufanyika kila siku ya Jumanne, ulifanyika mapema zaidi kumwezesha Bw Mugabe kwenda Libya kuhudhuria mkutano wa viongozi wa mataifa wa African Union.

Wakati Bw Mugabe akiwa nje ya nchi, kiongozi wa MDC, ambaye ni waziri mkuu Bw Morgan Tsvangirai huendesha vikao vya baraza la mawaziri.

Naibu kiongozi cha MDC amesema chama tawala kimeonyesha "dharau" kuhusu serikali ya muungano ya kugawana madaraka iliyoundwa Februari 2009.

Chama cha Zanu-PF "hakijaipokea MDC kama mshirika sawal", Makamu wa rais wa MDC, Thokozani Khupe alisema.

Alisema uamuzi wa kubadilisha ratiba ya kikao unaashiria " maamuzi ya upande mmoja, kukosa heshima, dharau na kukataa kutambua hali halisi na utaratibu wa makubaliano ya kisiasa", shirika la habari la AFP lilimnukuu akisema hivyo.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA