TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Thursday, April 1, 2010

Uwanja wa ndege kujengwa Holili, Taveta

4:42 PM

Uwanja wa ndege wa kisasa unatarajiwa kujengwa mpakani mwa Tanzania na Kenya katika maeneo ya Holili na Taveta kama njia ya kuimarisha utalii na kukuza biashara katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Balozi wa Kenya nchini, Mutinda Mutiso, alisema hayo wakati juzi akizungumza na wawekezaji na wadau mbalimbali mjini hapa juzi usiku.

Mutiso alisema uwanja huo utajengwa kilomita saba kutoka Holili kuelekea Taveta nchini Kenya.

“Zabuni imekwishatolewa kwa Serikali ya Kenya ili kumpata mkandarasi mahiri atakayejenga uwanja huo,” alisema.

Alisema uwanja huo ambao umepangwa kugharimu Sh. bilioni 10 za Kenya, utafungua milango na kuvuta watalii wengi katika ukanda huo.

Aliongeza kuwa awamu ya kwanza ya mradi wa ujenzi wa kiwanja hicho, inatazamiwa kumalizika miaka miwili ijayo na ya pili itachukua muda wa miaka mitatu.

Balozi huyo, alisema mikoa mitano ya Arusha, Kilimanjaro, Tanga, Manyara na Singida itanufaika kutokana na ujenzi wa uwanja huo.

Kwa mujibu wa Mutiso, ndege zitakazokuwa zinabeba watalii kutoka Amerika na Ulaya zitaruka moja kwa moja hadi katika uwanja huo ili kujionea vivutio vya utalii kama vile Mlima Kilimanjaro na mbuga za taifa za wanyama.

Alisema lengo la kujenga uwanja huo ni kuinua hadhi ya vivutio vya utalii katika Hifadhi ya Mkomazi kwa upande wa Tanzania na mbuga za wanyama za Tsavo na Amboseli nchini Kenya.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA