
Katika hotuba yake mjini Oslo, Obama alitetea wajibu wa Marekani katika vita vya Afghanistan, akisema kwamba nguvu za kijeshi zaweza kuleta amani ya kudumu.
Alisema amepewa tuzo hilo mapema ukilinganinishwa na watu wengine walioshinda tuzo hilo kabla yake.
Akizungumza kwa unyenyekevu, alisema wengine walistahili zaidi. Bw Obama pia alizungumzia vita viwili vinavyoongozwa na Marekani, akisema kuwa anafahamu kabisa gharama za vita hivyo.
Bw Obama alishinda tuzo hiyo mwezi Oktoba mwaka huu "kwa jitihada zake za kipekee kuimarisha diplomasia ya kimataifa na ushirikiano katika ya watu".
Sherehe hizo za siku ya Alhamisi katika mji mkuu wa Norway zilifanyika siku chache baada ya Bw Obama kutangaza kuongezwa kwa wanajeshi zaidi 30,000 kwenda nchini Afghanistan.
0 comments:
Post a Comment