Sunday, December 20, 2009

'Inasikitisha''Ajali ya Mohamed Trans: Simulizi za mikosi ya familia za zizimisha


SIMANZI, vilio na majonzi jana vilitawala katika Kijiji cha Mamba Kotela wakati wa mazishi ya ndugu sita wa familia moja ya Maleko waliofariki juzi wakienda katika harusi ya Egbert Maleko iliyokuwa ikitarajiwa kufanyika leo.

Ndugu hao Geofrey Maleko (70) mkazi wa Mbezi, James Maleko (32) na mtoto wake Mary James (6), Teoflas Maleko (42) na mkewe Grace Maleko (42) ambao ni wakazi wa Tabata Kisukuru pamoja na baba mdogo wa bwana harusi, Martin Maleko (68) mkazi wa Tabata na Johnson Moshi (14).


Ndugu hao walizikwa katika eneo moja la shamba la familia ya Maleko ambapo kijana Johnson Moshi alizikwa pembeni kidogo na eneo walilozikwa wenzake kwa maelezo yaliyotolewa na familia hiyo kuwa ni mtoto wa upande wa wajomba.


Akizungumza kwa niaba ya ukoo wa Maleko, Rumisha Maleko aliwaomba viongozi wa dini na serikali kuwa karibu na kijana wao ambaye alitarajiwa kufunga ndoa iliyotarajiwa kwenda sanjari na sherehe za kipaimara za watoto wao.


Alisema kijana huyo ana wakati mgumu kwa sasa kwani mwaka jana alipatwa na matatizo baada ya kuvamiwa na majambazi katika duka lake ambapo alifanikiwa kuwaua kwa kuwapiga risasi.


Hata hivyo wiki moja baada ya tukio la kuua majambazi hao, wakati mke wa kijana huyo akiwa nyumbani kwake, alisikia mlio wa bomba la gari la kutolea moshi uliomshtua na kufariki dunia papo hapo kwani alifikiri ni majambazi wamekuja tena kumdhuru.


Kutokana na tukio hilo kijana huyo aliamua kumtafuta binti mwingine kwa ajili ya kufunga ndoa ambapo wakati wakiwa katika hatua za mwisho ndipo ikatokea ajali hiyo na kuwapoteza ndugu zake saba huku wengine wakiwa katika hali mbaya katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC.



Akizungumza katika ibada ya Mazishi iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania Dayosisis ya Kaskazini Usharika wa Kimangaro Mamba, Askofu wa Dayosisi hiyo, Dk. Martin Shao alisema kuwa msiba huo haujagusa kanisa tu wala familia bali umegusa Taifa zima.


Alisema kuwa pamekuwepo ajali nyingi za mara kwa mara ambazo hupoteza maisha ya watu wasio na hatia kutokana na kukosekana kwa hekima na uzembe na wala si kwa mipango ya Mungu.


"Ajali nyingi zinatokana na uzembe wa watu wanaopenda kuharakisha mambo, madereva wetu wangekuwa makini na waangalifu na wakatembea kwa mwendo unaokubalika, ajali hizi zisingejitokeza na wala tusingepoteza maisha ya watu wengi kwa ajali za mara kwa mara," alisema.


Aidha alisema vifo vingi husababishwa na watu wasio na hekima wenye kutumia dawa za kulevya na nguvu za giza lakini kama yakipunguzwa mambo hayo, pakawepo hekima ambayo itaokoka roho za watu wengi.


Alisema Mkoa wa Kilimanjaro utafanya maombi Januari 2010 yatakayowashirikisha wachungaji na watumishi kutoka ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kuombea Taifa na Bara la Afrika kwa ujumla ili kuondoa maovu na kurejesha hekima iliyopotea.


Kwa upande wake mchungaji aliyekuwa akiongoza ibada ya mazishi, Rodrick Mlay aliwataka wafiwa kuwa na roho za subira wakimuomba Mungu na kuitaka serikali kuichunguza kamapuni ya Mohamed Tras ambayo basi lake ndiyo chanzo cha ajali hiyo.


“Yamesemwa mengi kuhusu ajali hii maana kampuni hii haina historia nzuri, haiwezekani kampuni moja ikamaliza watu wengi kiasi hicho, maana ni zaidi ya ajali tatu zimeshatokea na kuhusisha kampuni ya Mohamed Trans huku watu zaidi ya 100 wakipoteza maisha… kwa kweli tunapaswa kumuomba Mungu sana kwa hili,” alisema.


Akitoa salamu za Serikali, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Monica Mbega aliwataka wafiwa kutulia na kumuomba Mungu hasa katika kipindi hiki cha majonzi huku serikali ikiendelea kuchukua hatua zaidi kutokana na tukio hilo.


Mazishi hayo yalihudhuria viongozi mbalimbali wa vyama, serikali na dini akiwemo, Mbunge wa Vunjo Aloyce Kimaro, Mbunge wa Viti Maalum mkoani Kilimanjaro, Shally Raymond, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, Vicky Nsilo Swai, na Kamanda wa Polisi mkoani humo, Lucas Nghoboko.



Naye Lucy Lyatuu anaripoti kuwa jirani wa familia hiyo aliyepo Tabata Kisukuru Dar es Salaam, Baraka Elias alisema walipata tarifa za msiba huo juzi majira ya saa 12:30 jioni.


Alisema wanandugu wengine waliokuwa wamebaki Dar es Salaam walipigiwa simu na kupewa ujumbe kuhusu ajali hiyo kwa kuwa muda wote wa safari walikuwa wakipeana taarifa za kilichokuwa kikiendelea katika msafara huo.


Elias alisema safari ya wanandugu hao ilipangwa kufanyika Jumatatu Desemba 14, 2009, lakini kutokana na kuhitajika kuendelea kukusanya michango zaidi ya harusi na marekebisho madogo ya gari walilosafiria ilibidi kuahirisha safari na kusogeza mbele hadi juzi.


Hata hivyo, Elias alisema katika harusi waliyokuwa wakihudhuria bwana harusi mtarajiwa Egbert Maleko alikuwa akifunga harusi hiyo kutokana na aliyekuwa mke wake wa awali kufariki, hivyo kuruhusiwa kuoa mke mwingine.


“Wanandugu wote waliobaki Dar es Salaam wameondoka juzi saa 3:00 usiku mara baada ya kupatiwa taarifa ya msiba ili kuwahi maziko ambayo yanatarajiwa kufanyika leo (jana).


“Hapa kwa Toeflas tumebaki vijana wawili wa kazi kwa ajili ya kulinda usalama wa makazi haya,” alisema Baraka ambaye ndiye aliyebaki katika nyumba Toeflas Maleko.



The Best-Performing CEOs in the World



Steve Jobs

Reliance Industries chairman Mukesh Ambani has been ranked the fifth best performing CEO in the world by the prestigious Harvard Business Review (HBR) with Apple’s Steve Jobs occupying the top spot.

Mukesh Ambani is the lone Indian to feature in this list among the top 50 CEOs of the world.


Ahead of Ambani, the other top CEOs are, Job, Yun Jong-Yong of Samsung Electronics, Russian energy firm Gazprom's Alexey Miller and John Chambers of Cisco Systems.


The likes of Jack Welch, Warren Buffett, Larry Ellison and Bill Gates have not found a place in the list as HBR considered only CEOs who assumed the job between January 1995 and December 2007 period.


Ambani is also ranked number two among the top 10 emerging market CEOs with Miller at the top. K.V. Kamath of the ICICI Bank is the other Indian in the list, who is at number 9.


The HBR report said it ranked CEOs of large publicly traded companies in a study conducted over 2,000 CEOs worldwide. The entire group represented 48 nationalities and companies based in 33 countries. "On an average, the top 50 CEOs increased the wealth of their shareholders by $48.2 billion," it said. "They delivered a total shareholder return of 997 percent during their time in office. That translates into a spectacular annual return of 32 percent," it added.


The HBR put Ambani in the list of "up-through-the-ranks leaders" along with the Samsung boss Yun Jong-Yong.


"Among the up-through-the-ranks leaders on our list are Yun Jong-Yong, who joined Samsung straight out of college and worked there 30 years before becoming CEO, and Mukesh Ambani, who joined RIL in 1981, when it was still a textile company run by his father.


Ranking Steve Jobs as the top CEO in the world, HBR said, "These CEOs may not all be household names, but here's an objective look at who delivered the top results over the long term."


It also said that Jobs delivered a whopping 3,188 percent industry-adjusted return, which is about 34 percent compounded annually after he rejoined Apple as CEO in 1997. From thenuntil the end of September 2009, Apple's market value increased by $150 billion. Yun Jong-Yong was second, who ran South Korea's Samsung Electronics from 1996 to 2008

Saturday, December 19, 2009

UN yaafiki makubaliano ya Copenhagen


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amefurahishwa na mpango wa Marekani wa hali ya hewa mjini Copenhagen na kuuita "mwanzo muhimu".

Alikuwa akizungumza baada ya wajumbe kupitisha muswada unaotambua makubaliano hayo, ambayo Marekani iliyafikia pamoja na mataifa muhimu ikiwemo China na Brazil.

Lakini Bw Ban amesema makubaliano hayo ni lazima yafanywe kuwa sheria itakapofika mwaka ujao.

Mapema mkutano huo ulionekana kusambaratika baada ya baadhi ya mataifa masikini kuukataa mpango wa kupambana na mabadiliko ya hali ya hali ya hewa.


Friday, December 18, 2009

Obama, other leaders meet again at climate summit


COPENHAGEN – President Barack Obama and world leaders are holding another impromptu meeting in search of a climate deal.

Obama spokesman Robert Gibbs said Friday that Obama was meeting behind closed doors with the leaders of Australia, the United Kingdom, France, Germany and Japan. Also participating in the talks were developing countries Ethiopia, Bangladesh and Colombia, among others.

China and Russia, both seen as key participants in the U.N. sponsored climate talks, also were present.

It was the second meeting of the day for the group. Obama headed into the first meeting right after arriving in Copenhagen. Chinese Premier Wen Jiabao skipped the high-level meeting a second time and sent another envoy instead.here


TAWI JIPYA LA EXIM LAZINDULIWA

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam William Lukuvi (kushoto), Mwenyekiti wa Exim Benki , Yogesh Manek na Mkurugenzi Mtendaji wa Exim Benki Sabetha Mwambenja wakifurahi baada ya kuzindua tawi la Ubungo jana. Wa pili kutoka Kulia ni Meneja wa Benki hiyo, Nancy Huggins.(Na Mpigapicha Wetu)

Ratiba ya klabu bingwa Ulaya
Ratiba ya timu 16 zinazocheza ligi ya klabu bingwa barani Ulaya imetolewa hii leo. Michezo ya kwanza itafanyika Februari 16 mwaka 2010.

Ratiba yenyenyewe ni kama ifuatavyo:

Inter Milan Kucheza na Chelsea
Lyon kucheza na Real Madrid
AC Milan kucheza na Manchester United
Olympiakos kucheza na Bordeaux
FC Porto kucheza na Arsenal
CSKA Moscow kucheza na Sevilla
Stuttgart kucheza na Barcelona, na
Bayern Munich kucheza na Fiorentina



Askofu Muasi apokonywa Upadre


Kanisa katoliki imempokonya upadre askofu wake wa zamani nchini Zambia Emmanuel Milingo kama hatua ya kumzuia kuwatawaza makasisi wanaoishi katika ndoa.

Milingo aliasi maadili ya kanisa katoliki ya maisha ya useja. Makao makuu ya Vatican yamesema hatua yake ni kuhakikisha wanaotawazwa na Milingo hawatambuliwi na kanisa hilo.

Askofu huyo wa zamani alitengwa na kanisa hilo mwaka wa 2006.Msemaji wa Vatican Federico Lombardi amesema Milingo alistahili kufukuzwa, baada ya kuendelea kuwatawaza maaskofu licha ya kutengwa na kanisa hilo.

Aliongeza kutawazwa kwa makasisi wanaoishi katika ndoa ni kinyume na maadili ya imani hiyo na kunatishia kuzua mgawanyiko katika kanisa katoliki.


new year's eve bash @ canton


Tired of bringing in the new year in the same way every year?
Make this year a year to remember!

The Tanzania Associan of Canton
presents,
a New Year bash at Lollies Banquet hall of Belden Village.
$5.00 cover charge at the door. Food, drinks, and fun!
Music by DJ Kvelli of Columbus. Rap, Hip-Hop, and much more!
Call 330-418-6401 or 330-575-7148 for V.I.P and info.

Thursday, December 17, 2009

msiba greece


JUMUIYA YA WATANZANIA NCHINI GREECE INATANGAZA MSIBA WA NDUGUYETU MPENDWA BW.SAIDI MACHALA KILICHOTOKEA JUZI TAR 14/12/09 KTK HOSPITALI YA SUTIRIA MWENYE NGUO NYEUSI AMBAE ALIKUA KIPA WETU NO 1.MPANGO WA KUMSAFIRISHA MWILI WA MAREHEMU KWENDA NYUMBANI TANZANIA KWA MAZISHI UNAENDELEA.MWENYEZIMUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHARI PEMA PEPONI AMMIN.KWA LAZAIDI LITAKALOENDELEA TUTAPEANA TAARIFA,
BY HAJIEZ.

JK AKIWA MAABARA

Rais Jakaya Kikwete, akitazama vijidudu vya maradhi kupitia mashine iliyopo kwenye maabara ya kisasa ya Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) jijini Dar es Salaam

Wednesday, December 16, 2009

Tanzanian scientist invention recognised by American Engineers

Vituo 13 vya mafuta vyakamatwa Dar


Wakala wa Vipimo na Mizani Tanzania, wamekamata mashine 13 za kuuza mafuta ya petroli Dar es Salaam zilizogundulika kufanyiwa udanganyifu, ili kuwaibia wateja.

Operesheni iliyoendeshwa jana, katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, ilibaini mashine hizo katika vituo vitatu, na kuvipiga marufuku kuendesha biashara hiyo.

Kwa mujibu wa mkuu wa operesheni hiyo Wilbroad Kimaro, msako huo umelenga kuhakikisha kuwa watu wanapata huduma zinazolingana na fedha wanayotoa.

Hivi karibuni Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji, Ewura, Haruna Masebu, alibainisha kuwa zaidi ya asilimia 70 ya vituo vyote 900 nchini vinajihusisha na udanganyifu katika biashara hiyo.

Wahamiaji Waafrika wakwama Iraq

Shirika la kimataifa linaloshughulikia maslahi ya wahamiaji, IOM linasema mamia ya wahamiaji kutoka Afrika na Asia wamekwama nchini Iraq.

Wahamiaji hao wanasumbuka kwani hawana fedha za kuwasaidia kuondoka nchini humo.

Msemaji wa shirika hilo Jemini Pandya amesema wanatafuta dola milioni mbili unusu kuwasaidia wahamiaji 700 wanaondelea kuhangaika nchini Iraq.

Amesema kwa miaka sita shirika lake limekuwa likiwasaidia wahamiaji 7,000 lakini ni 32 pekee walioweza kuokolewa mwaka huu.

Ameongeza wahamiaji wengi walihadaiwa kusaini mikataba ya kazi zisiszo za kweli nchini Iraq.

Wengi hupokonywa hati zao za kusafiria na hufanya kazi katika mazingira mabovu.

Mwafrika aweka historia Australia

Mkimbizi kutoka Sudan ameandika historia kwa kuwa Mwafrika wa kwanza kujiunga na ligi ya kulipwa ya mpira wa miguu ujulikanao kama Australian Rules.

Majak Daw mwenye umri wa miaka 18 amesajiliwa na mojawapo ya vilabu maarufu ya, North Melbourne.

Anatumai kuwa mafanikio yake yatawahamasisha Waafrika wengine waliohamia Australia kushiriki katika mchezo huo.

Majak Daw na familia yake walikimbia vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sudan alipokuwa na umri wa miaka tisa na aliwasili nchini Australia mwaka 2003 baada ya kuishi nchini Misri.

Kijana huyo mrefu alianza kucheza Australian Rules Football miaka minne tu iliyopita.

Ubaguzi umemuandama Majak tangu ajiunge na ligi hiyo lakini anasema matusi anayotupiwa viwanjani yanamsaidia kumtia moyo zaidi.

ruge mutahaba alonga

JK akiwa na Ruge Mutahaba wakati wa shoo ya THT jijini Dar karibuni
SWALI: Ruge mutahaba ni nani?

RUGE: Nimezaliwa Brooklyn New York Marekani mwaka 1970, Primary School nimesoma Arusha School standard 1 hadi 6, kisha nikahamia Mlimani Primary School maeneo ya Chuo Kikuu Dar es Salaam na ndipo nilipomaliza darasa la saba. Kisha nikasoma Forodhani Secondary School form 1 – 4, baadae Pugu High School 5 na 6. baada ya hapo nikarudi Marekani ambako nikaenda kusoma San Jose University California ambako nikachukua BA in Marketing na pia nikawa nakachukua BA in Finance, kozi zote nilisoma ndani ya miaka 5, kind of 2 courses at the same time. Baada ya hapo nikarudi tena Tanzania.

SWALI: Nini kilichotokea hadi ukajikuta uko cloudz FM.

RUGE: Wakati nipo Marekani, Joseph Kusaga alikuwa na disco, Clouds Disco, mimi nikawa supplier wake wa vifaa mbalimbali vya music, then hapo tuka-build good friendship. Sasa, niliporudi Tanzania baada ya kumaliza masomo yangu, Joseph Kusaga akanishawishi sana nibaki kutokana na opportunity zilizokuwepo za kuanzisha Radio na kuipeleka katika level nyingine kabisa, ndipo nilipojikuta nipo Clouds Entertainment.

SWALI: Tuambie kuhusu THT.
RUGE: Kama Clouds Entertainment tuliamua kuanzisha kampuni ya management ya wasanii ambayo tuliita Smooth Vibes ambayo ndiyo kampuni iliyowatoa wanamuziki kama Lady Jay Dee, Ray C na wengineo. Unajua utakuta kati ya wasanii watano, only mmoja au wawili wana-survive na suddenly utakuta msanii alikuwepo then kapotea. Hii inatokana na kutokuwa na foundation nzuri. Hivyo nikaona ni bora nianzishe House of Talents ambayo sasa kupitia hiyo, tukawa tunawafundisha wasanii misingi ya muziki, kumfundisha msanii how to Manage Industry, Vocal Coaching, Music Business, Music Instrumentation, Dance Classes na kadhalika.
Nikagundua kuwa unakuta msanii anaenda kwenye show lakini performance inakuwa mbovu na pia ili msanii aweze ku-last longer kwenye game anatakiwa ajue dancing. Ndio maana THT tukawa na dance classes. THT imewatoa wasanii wengi kama Maunda Zorro, Mwasiti, Marlaw, Barnaba na wengineo. THT hadi sasa ina miaka minne.

Kupata intavyuu nzima

Mkutano wa mazingira waanza upya

Mazungumzo kwenye mkutano wa kilele juu ya mazingira yameanza tena baada ya matakwa ya nchi changa kuafikiwa.

Mazungumzo ya faragha yataendeshwa kwa njia mbili kama Mataifa makuu yanavyotaka kwa kuzingatia makubaliano ya Kyoto.

Hata hivyo mazungumzo ya kina yanaanza usiku wa leo ingawa bado kuna kazi kubwa endapo makubaliano yoyote yatafikiwa.

Wajumbe wanatafakari maelezo ya mapendekezo mapya yaliyotolewa mapema leo kwenye mkutano.

Kufuatia hatua ya Mataifa machanga kuususia mkutano hapo jana jumatatu ilibidi kufanyike vikao vya ziada usiku kucha ili wajumbe waweze kufidia mda uliopotea.

Tuesday, December 15, 2009

Watakaopandisha nauli kulimwa faini 200,000/-


Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini nchini (Sumatra), imetoa ufafanuzi kuhusu adhabu itakayowakumba wamiliki wa mabasi ya mikoani watakaofanya makosa ya kupandisha nauli kiholela, kwa kusema kwamba, yatatozwa faini ya Sh. 200,000.

Meneja wa Mawasiliano wa Sumatra, David Mziray, alisema jana kuwa wanaendelea na mikakati ya kujiimarisha kutekeleza kampeni ya kuwadhibiti wanaotenda makosa hayo.

“Kwa jumla, makosa yote ya nauli adhabu yake ni faini ya sh. 200,000 na si sh. 100,000 kama ilivyoripotiwa jana,” alisema Mziray.

Sumatra imetoa onyo hilo zikiwa zimesalia wiki mbili kuingia vipindi vya Sikukuu za Krismas na Mwaka Mpya, ambavyo baadhi ya wamiliki na mawakala wa kampuni za mabasi hayo, huvitumia kupandisha nauli kwa abiria pamoja na mizigo.

Juzi, Mziray alikaririwa akisema kwamba, kampeni ya kudhibiti mabasi hayo dhidi ya vitendo hivyo, inatarajiwa kuanza kufanywa na Mamlaka hiyo wiki hii nchini kote.

“Napenda kutumia nafasi hii kuwaonya wamiliki wa mabasi watakaojaribu kupandisha nauli kinyume na ile inayotambuliwa na Sumatra kwamba, watachukuliwa hatua, ikiwa ni pamoja na kutozwa faini. Na abiria watarejeshewa kiasi cha fedha kilichozidi katika nauli halali,” alisema Mziray.

Aliongeza kuwa wamekuwa makini dhidi ya watu wanaopandisha nauli za mabasi kiholela na kwamba, walianza kujipanga kudhibiti kero hiyo miaka miwili iliyopita, kwa vile imekuwa ikifanywa kwa nia mbaya ya kuwakomoa wananchi.

Alisema mkakati huo umekuwa ukitekelezwa na Sumatra katika vituo mbalimbali vya mabasi, ambavyo vimekuwa sugu katika kutumiwa na wajanja hao kuendesha vitendo hivyo, kikiwamo Kituo Kikuu cha Mabasi cha Ubungo (UBT), jijini Dar es Salaam na cha Kibaha, mkoani Pwani.

Kutokana na hali hiyo, aliwataka abiria kuchukua tahadhari kwa kuhakikisha wanajiorodhesha mapema kwenye kitabu cha abiria (booking) na kukata tiketi kwenye ofisi za kampuni za mabasi ili kuepuka kulanguliwa tiketi na wajanja wachache walioweka mawindo yao kwenye vituo hivyo.


DECI wakwaa balaa jipya

Viongozi wa ile taasisi ya kupanda na kuvuna fedha ya Development Enterprenureship Community Initiative, DECI, inayodaiwa kuendesha shughuli za upatu kinyume cha sheria za nchi, wamekwaa kesi mpya.

Hati ya mashtaka ya kesi hiyo, inawataja washitakiwa kuwa ni Dominic Kigendi, Jackson Sifael Mtalesi, Timotheo Ole Loiting'ye na Samwel Mtalesi.

Wote wanashitakiwa kwa kosa la wizi.

Hati ya mashtaka inasema, watuhumiwa hao wakiwa wakurugenzi wa DECI Tanzania Ltd, kati ya Desemba Mosi na Desemba 8 mwaka huu, wakiwa mahali pasipojulikana, walikula njama kwa nia ya kuibia umma kiasi cha shilingi 118,440,000.

Katika kosa la pili, watuhumiwa wote wanadaiwa kuwa mnamo Desemba 8 mwaka huu, wakiwa katika Benki ya Standard Charterd tawi la Kariakoo, Ilala Jijini Dar es Salaam, kwa pamoja walikuwa na lengo la kuiba shilingi 118,440,000, mali ya kampuni ya DECI.

Hadi gazeti hili linakwenda mitamboni, watuhumiwa hao waliofikishwa kwenye mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu mapema asubuhi, walikuwa bado hawajapandishwa kizimbani.

Denti Dar ajilipua kwa risasi

Kijana mmoja mkazi wa Jijini Dar es Salaam, amekufa papohapo baada ya kujilipua kwa risasi leo asubuhi.

Kijana huyo amefahamika kwa jina la Idd Swaibu Hoza, 28, mkazi wa Mbezi Ndumbwi.

Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Ndumbwi, Bw. Salustian Cashimiry Kimaro ameliambia gazeti hili leo asubuhi kuwa, tukio hilo limetokea mishale ya saa 3:00 asubuhi, nyumbani kwa wazazi wa mwanafunzi huyo maeneo ya Mbezi.

Akisimulia tukio hilo, Bw. Kimaro amesema kijana huyo alitarajia kuanza masomo ya elimu ya juu hivi karibuni, baada ya kumaliza kidato cha sita katika shule ya sekondari ya Benjamini Mkapa.

Amesema bunduki aliyotumia ni aina ya Shortgun na hutumiwa na mlinzi anayelinda nyumbani kwao.

Amesema mlinzi huyo aitwaye Eliud Seleman Ntaita kila siku anapomaliza lindo lake, huhifadhi silaha hiyo chini ya uvungu wa kitanda nyumbani hapo na kisha huondoka zake.

Bw. Kimara amesema hadi sasa sababu za kijana huyo kujilipua bado hazijafahamika.

CHANZO: ALASIRI

Mashabiki wazidi kupoteza imani kwa Maximo


Kilio cha mashabiki wengi wa soka Tanzania kutaka kocha wa timu ya taifa, Marcio Maximo kuachia ngazi, kimezidi baada ya timu ya Tanzania bara kuvurunda katika mashindano ya CECAFA.

Kabla ya kuanza kwa michuano hiyo iliyomalizika Jumapili mjini Nairobi,Maximo alitamba kwamba angewaziba midomo watu wanaohoji uwezo wake wa kuifundisha timu hiyo kwa kupata mafanikio.

Mashabiki hao wamezidi kufura hasira baada ya timu yao kukosa nafasi za juu, pale ilipojikuta ikishika nafsi ya nne baada ya kuchapwa na ndugu zao wa Zanzibar Heroes goli moja kwa bila.

Baadhi ya wadau wanadai kocha huyo Mbrazil hana jipya katika kuifundisha timu hiyo na kumtaka aachie ngazi.


Matumaini ya kukabiliana na HIV yadidimia


Dawa maalum ya kupaka ambayo ilikusudiwa kuzuia maambukizi ya ukimwi haijafanikiwa, baada ya majaribio makubwa ya kimataifa kuwahi kufanyika.

Baraza la utafiti wa matibabu nchini Uingereza ambalo liligharamia majaribio hayo katika nchi za Afrika, limeelezea matokeo yake kuwa ya kuvunja moyo baada ya kuwepo na matumaini makubwa na vile vile kuwekeza fedha nyingi katika mradi huo.

Zaidi ya wanawake elfu tisa katika nchi nne za Kusini mwa jangwa la Sahara walishiriki katika majaribio hayo.
Wanawake hao walipewa krimu ya kupaka kwenye sehemu zao za siri iitwayo PRO 2000 ambayo ilitakiwa kupakwa kabla ya kujamiiana.

Barani Afrika zaidi ya asilimia 60 ya walioambukizwa virusi vya HIV na Ukimwi ni wanawake na wengi wao waliambukizwa kutokana na wapenzi wao waasharati.

Majaribio mengine yanaendelea kufanywa lakini Dkt. Sheena McCormack wa baraza la utafiti wa matibabu la Uingereza anasema matokeo "yanavunja moy

Mwanadiplomasia atimuliwa Tanzania

Mwanadiplomasia mmoja kutoka Canada aliyemtemea mate polisi na mwandishi wa habari nchini Tanzania anarejeshwa kwao.

Balozi wa Canada Robert Orr aliitwa na waziri wa mambo ya nje wa Tanzania kuzungumiza tukio hilo wiki iliyopita.

Bw Orr alisema, "Kwa faida ya nchi zote mbili, afisa huyo wa Canada ataondoka nchini Tanzania haraka iwezekanavyo."

Hata hivyo, mwandishi wa habari aliyetemewa mate na mwanadiplomasia huyo amesema bado anataka kuchukua hatua za kisheria.

Jerry Muro, anayefanya shirika la habari la taifa la TBC ameliambia gazeti moja la HabariLeo nchini humo , "Haki lazima itendeke. Kumrejesha ni hatua moja tu, lakini haimaanishi kwamba yamekwisha. Nitakwenda polisi kuhakikisha wanashikilia hati yake ya kusafria."

Monday, December 14, 2009

Baada ya kasheshe Woods apumzika Golf


Tiger Woods ameamua kupumzika kwa muda usiojulika kucheza gofu ili aweze kukabiliana na matatizo yanayoizonga familia yake hivi sasa.

Katika taarifa aliyoitoa kupitia mtandao wake amesema anafahamu namna alivyowakasirisha wapenzi wa mchezo wa gofu kutokana na kukosa uaminifu alikoisababishia familia yake.

Mcheza gofu huyo anayeshikilia nafasi ya kwanza duniani anajaribu kutengeza pale alipoharibu na ameomba faragha kwa familia yake.

Wadhamini wakubwa wa Woods kampuni ya vifaa vya michezo ya Nike imesema itaendelea kufanya kazi nae, lakini wakala wake amesema ni mapema mno kuzungumzia athari za kibiashara anazofanya.

Kupitia mtandao wake Woods ameomba msamaha na kutaka asamehewe.

Wakenya 20 wapigwa marufuku Uingereza.


Uingereza imewapiga marufuku zaidi ya wakenya 20 ikiwa nipamoja na maafisa wa ngazi za juu kuitembelea kutokana na madai ya ufisadi .

Balozi wa Uingereza mjini Nairobi amesema kwamba marufuku hiyo imechukuliwa kama hatua ya mwisho kuhakikisha kuwa watu binafsi wanaohusishwa na ufisadi wanafanyiwa uchunguzi na kushtakiwa nchini Kenya.

Hatahivyo amesema kuwa hakuna afisa wa ngazi za juu serikali aliyeshtakiwa kikamilifu katika mahakama ya Kenya, amesema serikali ya Kenya imekuwa ikipuuza maombi ya wachuunguzi wanaotaka maelezo zaidi kuhusu washukiwa.


Berlusconi hit in the face

The Italian Prime Minister Silvio Berlusconi was today hit in the face with a metal object by a member of public. Berlusconi was addressing a rowdy crowd in Milan.
Berlusconi is reported to have sustained facial lacerations and suspected broken teeth. He was rushed to the hospital where he will spend the night under observation.

Berlusconi, who is also the owner of the football team AC Milan, has a vast media empire in Italy. He has been the Prime Minister of Italy three times since 1994.

Berlusconi has been attracting the media attention for all wrong reason, he is well known for his gaffes, off the cuff remarks, corruption and sex related scandals. His wife is currently seeking a divorce amid allegations of "transgressions" with a young girl.

New song Albino fulani ft Sugu, Belle 9 and MwanaFA

Albino Fulani

He goes by the name of Albino Fulani who recently organized an outstanding benefit concert to raise funds to help kids with albinism by providing sun blocks to prevent skin cancer who also participated in Baby Powder the movie has just released a HIT new single “NAFASI” Featuring Sugu and Belle 9 on chorus and Mwana FA on the 2nd verse. The song which was officially released at Friday night show on East Africa Television (EATV) song talks about things they will do if they were given a chance.

Enjoy!!!!
www.babkubwa.com
www.babkubwa.ning.com
www.bongomusic.wordpress.com

bonanza la michezo kusherehekea Uhuru Day lafana New Delhi

Mh_Balozi Mhandisi John Kijazi akifurahia kombe la ushindi ambalo timu ya Ubalozi wa Tanzania India ulishinda kabla hajalikabidhi kwa timu captain. Katika kusherehekea Uhuru wa Tanzania Jumuiya ya wanafunzi wanaosoma India na Ubalozi wa Tanzania nchini humo uliandaa bonanza la michezo nyumbani kwa balozi ambalo lilifana sana.
mbio za 'vipofu' zikikaribia kuanza
mashindano ya kula maandazi yanayoning'inia
shindano la kuvuta kamba kati ya timu ya
wanafunzi na wafanyakazi wa ubalozi. ngoma ilikuwa droo
kukimbia na ndimu
balozi akitoa mawili matatu kwa timu ya ubalozi kabla ya gemu

Mh Balozi Mhandisi John Kijazi akiwa Mwenyekiti wa Tasa Bi. Jennifer Sumi (kulia) na Makamu wa Rais Jane Balama wakishuhudia mchezo wa soka.
Timu kabambe ya wanafunzi kabla ya gemu
umoja na upendo kati ya wanafunzi na wafanyakazi wa ubalozi

Sunday, December 13, 2009

Miss Gibraltar is Miss World 2009

Miss Gibraltar Kaiane Aldorino has been named winner of the 2009 Miss World pageant in Johannesburg. Kaiane had also won the swimsuit round and was a favourite of the judges.

Miss Mexico, Perla Beltran Acosta, was the first runner up followed by Miss South Africa, Tatum Keshwar. Apparently, Miss South Africa was the hot favourite to win the crown.

Ex-Miss World and Bollywood actress Priyanka Chopra was one of the judges at the event. The coveted beauty pageant is in its 59th year presently and has received participation of ladies from 112 different nations round the globe.

India's Pooja Chopra failed to make it to the final round of seven competitors, dashing the hopes of many an Indian of getting the title back to the country.

Pooja had earlier made it to the semifinal round of 16 competitors on the basis of her Beauty With Purpose project on saving the girl child.

India has not won the title since 2000 when Priyanka Chopra brought the crown

Apart from her, India boasts of Miss Worlds like Reita Faria (1966), Aishwarya Rai Bachchan (1994), Diana Hayden (1997) and Yukta Mookhey (1999).

Saturday, December 12, 2009

Vigogo wapigana vikumbo harusi ya binti Lowassa


KIKWETE ATIA DOA BAADA YA KUSHINDWA KUTOKEA UKUMBINI, DK SHEIN, MWINYI, KARUME, NAHODHA, DK SALIM, WARIOBA, WATINGA

Ramadhan Semtawa

EDWARD Lowassa, ambaye alijiuzulu uwaziri mkuu kutokana na kashfa ya mkataba wa kifisadi kati ya kampuni ya Richmond Development (LLC) na Tanesco, juzi alitikisa Jiji la Dar es Salaam baada ya sherehe ya kumuaga bintiye anayeitwa Dk Anna kuvuta vigogo wengi akiwemo makamu wa rais, Dk Ali Mohamed Shein na rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi.

Sherehe hiyo kubwa iliyofanyika Desemba 8 mwaka huu kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, ilianza majira ya 12:30 jioni na kumalizika saa 7:30 usiku, lakini Rais Jakaya Kikwete alishindwa kuhudhuria na kutoa udhuru dakika za mwisho.

Wingi wa vigogo hao waliohudhuria sherehe hiyo unaweza kuzidi hata idadi ya vigogo waliohudhuria sherehe za miaka 48 ya uhuru wa Tanganyika zilizofanyika kesho yake kwenye Uwanja wa Uhuru.

Wakati mawaziri wa zamani na vigogo wengine hawakuhudhuria sherehe za uhuru, hali ilikuwa tofauti kwenye sherehe ya kumuaga binti Lowassa ambazo zilihudhuriwa na vigogo wengi wa CCM na serikali, ukiacha Rais Kikwete, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Spika wa Bunge Samuel Sitta na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe.hapa zaidi

DPP amvaa Dk Hoseah, ataka mdahalo majalada kesi za kifisadi

Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah ambaye jana alidai kuwa DPP amekalia kesi 60 tuhuma za rushwa

Mrembo wa Tanzania, (Miss Vodacom), Miriam Gerald

Mrembo wa Tanzania, (Miss Vodacom), Miriam Gerald ambaye leo atapanda jukwani nchini Afrika ya kusini kusaka taji la urembo la Dunia

Gavana Kwan-Yong Kim wa korea ikulu

Rais Jakaya Kikwete (kulia) akimkaribisha Gavana Kwan-Yong Kim kutoka Jimbo la Gyeongsangbuk-do, Jamhuri ya Korea wakati gavana huyo alipomtembelea Rais, Ikulu Dar es Salam

10 YEARS ANNIVERSARY

THE LATE WILSON MLEKIO LAWERE
It is 10 years since you were suddenly called by our almighty God to his Eternal love on 12th December 1999. Your love, kindness, wisdom and caring is deeply missed by your lovely wife AMINI LAWERE, your children HAIKA, ROBERT, ANDREW,ANNA, Staff and Management of MBEZI GARDEN HOTEL.
The legacy you left to us on love, education, courage, hardworking and God loving will live with us for ever.

We thank God for your life that made you shining within the family and beyond. We will continue to fondly love, remember and treasure your life here.

We will have a thanksgiving service this Sunday, 13th December 2009 at 7:00am
Mbezi Beach Lutheran Church.


Friday, December 11, 2009

Wito wa kuhalalisha ukahaba India


Mahakama ya juu nchini India imeitaka serikali kutafakari hatua ya kuhalalisha biashara ya ukahaba ikiwa haiwezi kuikomesha.

Mahakama hiyo imesema ikiwa serikali itahalalisha biashara hiyo, makahaba huenda wakarebisha tabia yao huku biashara ya ulanguzi wa wanawake ikizuiwa.

Matamshi ya mahakama yamejiri wakati ikisikiliza kesi kuhusu biashara ya ulanguzi wa watoto iliyofikishwa mahakamani na shirika lisilo la kiserikali.

Ukahaba umepigwa marufuku nchini India lakini biashara hiyo imenawiri katika baadhi ya miji. Kuna takriban makahaba milioni mbili nchini India.

Mkutano wa mazingira wakabiliwa na kibarua


Viongozi wa Muungano wa ulaya wanakabiliwa na kibarua kigumu kuhusu kiwango cha pesa watakachotoa kwa hazina ya kimataifa kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya anga.

Viongozi wa Uingereza na Ufaransa, waziri mkuu Gordon Brown na rais Nicolas Sarkozy wanaokutana Brusselas, wamesema nchi zao zitatoa kima cha dola bilioni moja nukta tano kutumika kwa miaka mitatu.

Viongozi hao wamesema ni sharti mkutano wa Copenhagen uidhinishe kile wametaja kuwa hazina ya ufunguzi kusaida nchi maskini kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya anga.

Wamesema mkataba wowote utakoafikiwa sharti utimizwe katika muda wa miezi sita na sharti uruhusu kuongezwa mdaada hadi mwaka 2020.


Tanzania yaunda baraza la makosa ya jinai

Tanzania imezindua baraza la taifa litakaloshughulikia masuala ya makosa ya jinai, kwa lengo la kupunguza mlundikano wa kesi kwenye mahakama za nchi hiyo.

Serikali imelitaka baraza hilo kubuni mikakati madhubuti ikiwa ni pamoja na kuwa na ratiba maalum ya kumaliza kesi za jinai ambazo zimechukua muda mrefu mahakamani bila kumalizika.

Mapendekezo mengine yaliyotolewa na serikali katika kukabiliana na tatizo hilo ni pamoja na mahakama za Tanzania kuwatumia mahakimu wa heshima ama mahakimu ambao wamepata ruhusa kusikiliza kesi za mahakama kuu kwa kutumia sheria zilizopo.

Nusu wafeli mtihani darasa la saba,445,954 waenda kidato cha kwanza

Waziri wa Elimu na Mafunzo, Profesa Jumanne Maghembe akisisitiza jambo wakati alipokuwa akitoa taarifa ya matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya Msingi kwa mwaka 2009, Dar es Salaam.

Tanzanian scientist excel in the UK as world leaders focus on climate change

Mzungu aliyemtemea mate trafiki agoma kuhojiwa

Hussein Kauli na Tumsifu Sanga

AFISA ubalozi wa Canada aliyekamatwa na polisi Kanda maalum ya Dar es salaam kwa tuhuma za kumtemea mate askari wa usalama barabarni mwenye namba E 1653 koplo Samson, amegoma kuhojiwa.

Jean Touchatte (48) ambaye ni katibu muhtasi wa ubalozi huo nchini alikamatwa juzi saa 8:15 mchana maeneo ya Banana jijini Dar es Salaam baada ya kumtemea mate askari huyo akiwa kazini.

Kaimu Kamanda wa polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Charles Kenyela aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa afisa huyo amegoma kutoa maelezo polisi akishinikiza kwanza awepo balozi wake.

Alisema siku ya tukio mtuhumiwa huyo ambaye ni katibu muhtasi wa ubalozini hapo, alimtemea mate koplo Samson wakati akiongoza magari yanayotoka Ukonga kuelekea Uwanja wa ndege.

Kamanda Kenyela alisema sababu za kumtemea mate askari huyo bado hazijajulikana na mtuhumiwa anashikiliwa kwa uchunguzi zaidi.

Alisema baada ya Koplo Samson kutoa taarifa polisi gari hilo lilitangazwa askari waliokuwa doria walioanza kulifuatilia na alipofika barabara ya Nyerere karibu na Kamata gari hilo lilikamatwa na kupelekwa Makao Makuu ya Polisi trafiki Kanda maalum ya Dar es salaam.

Kamanda Kenyela alisema wakati mtuhumiwa anaendelea kuhojiwa walifika waandishi wa habari akiwemo Jerry Muro wa TBC kutaka kujua kwa nini katibu huyo alimtemea mate askari.

Wakati Jerry anamhoji naye alitemewa mate sehemu ya chini ya kidevu chake na kusambaa katika fulana yake aliyokuwa amevaa kitendo kilichosababisha mwandishi huyo kufungua jalada la shambulio CD/IR/4818/2009.

Kamanda Kenyela alisema fulana yenye mate imehifadhiwa kituo cha polisi kati wakati upelelezi unaendelea na kuongeza kuwa maelezo mengine kuhusiana na tukio hilo yatatolewa na Ispekta Jeneral wa Polisi Said Mwema.

Awali Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani, James Kombe, alisema suala hilo walimuachia Mkuu wa Jeshi la Polisi, Said Mwema, ungawa kwa mujibu wa taratibu atafikishwa mahakamani kulingana na uzito wa kosa linalomkabili.

Kombe alisema iwapo kosa lake litaonekana kuwa zito ataondolewa ulinzi wake na huenda hatimaye kufukuzwa nchini na kuwahakikishia wananchi kuwa haki itatendeka.

â€Å“Kwa mujibu wa taratibu huenda akafungiliwa mashitaka kuangalia uzito wa kosa alilofanya, iwapo kosa lake litaonekana kuwa zito ataondolewa kinga yake na kurudi nyumbani” alisema Kombe na kuongeza:

â€Å“Kwa kweli kitendo alichofanya ni kuidhalilisha nchi, hivyo naomba niwahakikishie wananchi kuwa haki itatendeka, na tayari huyo afisa yuko mikononi mwa polisi.”

Thursday, December 10, 2009

Obama apokea tuzo ya amani ya Nobel


Rais Barack Obama wakati akipokea tuzo ya amani ya Nobel, amesema Marekani lazima ionyeshe wajibu wa nia njema wakati inapopigana vita ambavyo ni lazima na vyenye kufuata sheria.

Katika hotuba yake mjini Oslo, Obama alitetea wajibu wa Marekani katika vita vya Afghanistan, akisema kwamba nguvu za kijeshi zaweza kuleta amani ya kudumu.

Alisema amepewa tuzo hilo mapema ukilinganinishwa na watu wengine walioshinda tuzo hilo kabla yake.

Akizungumza kwa unyenyekevu, alisema wengine walistahili zaidi. Bw Obama pia alizungumzia vita viwili vinavyoongozwa na Marekani, akisema kuwa anafahamu kabisa gharama za vita hivyo.

Bw Obama alishinda tuzo hiyo mwezi Oktoba mwaka huu "kwa jitihada zake za kipekee kuimarisha diplomasia ya kimataifa na ushirikiano katika ya watu".

Sherehe hizo za siku ya Alhamisi katika mji mkuu wa Norway zilifanyika siku chache baada ya Bw Obama kutangaza kuongezwa kwa wanajeshi zaidi 30,000 kwenda nchini Afghanistan.