TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Thursday, January 26, 2012

Mkuu wa polisi afukuzwa kazi Nigeria

2:14 PM
Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan, amemfuta kazi kamishna wa polisi kutokana na ongezeko la visa vya mashambulizi yanayotekelezwa na kundi la wanamgambo wa Kiislamu la Boko Haram.
Taarifa kutoka ikulu ya Nigeria imesema kuwa Hafiz Ringim amelazimishwa kwenda likizo ya lazima huku akisubiri kustaafu rasmi.
Hatua ya kumstaafisha mapema mkuu wa Polisi , wiki chache tu kabla ya kustaafu rasmi inaonyesha jinisi gani swala la Boko Haram limeitatiza serikali ya Goodluck Jonathan.
Baada ya mashambulizi ya hivi karibuni ya kundi hilo la Boko Haram serikali imekuwa ikishinikizwa kuchukua hatua madhubuti kukabiliana na hali hiyo.
Hivyo hatua ya kumtimua kazi mkuu wa polisi inaonekana kuwa ni njia mojawapo ya kuwafanya wa Nigeria wawe na imani na kikosi cha polisi cha nchi hiyo.
Ishara kuwa mkuu huyo wa polisi alikuwa amelemewa na kazi ni pale mshukiwa mkuu wa Boko Haram ambaye ana tuhumiwa kupanga mashambulizi katika kanisa moja na kusababisha vifo vya watu karibu 30 siku ya krismasi alipotoroka jela.
Mambo yalionekana kumlemea Hafiz Ringim, wakati alipotangaza kuwa atakabiliana vilivyo na kundi la Boko Harama hadi alimalize ,lakini siku chache baadaye kituo cha polisi kikashambuliwa na kundi hilo la Boko Haram.
Taarifa toka ikulu ya Nigeria inasema kuwa hivi karibuni kikosi kizima cha polisi kinatarajiwa kufanyiwa marekebisho ili kuimarisha utendaji kazi wake.BBC

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA