TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Tuesday, August 30, 2011

Kisoma cha Hitma pamoja na futari iliondaliwa na jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community Washngton DC

6:37 PM



Jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community jana jumapili  katika mwezi mtukufu wa Ramadhani ya 28, Aug 28, 2011  walifanikisha kusoma kisomo  cha kumuombea Marehemu Baba wa Dada yetu Jasmine Rubama, pamoja na kuwaombea jamaa zetu wote waliotangulia mbele ya haki, na  futari ilioandaliwa na jumuiya ya kiislamu Tamco Tuwasiliane, vile vile mgeni rasmami washuhuli hiyo alikuwa Mh. Balozi  Mwanaidi  Maajar kwenye ukumbi wa Hillandale  Local Park New Hampshire Avenue, Silver Spring, MD Nchini marekani.  


Ndugu jamaa pamoja na marafiki waliohudhuria katika kisomo pamoja na futari ilioandaliwa na  jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community kenye ukumbi wa Hillandale  Local Park New Hampshire Avenue,
Silver Spring Maryland.

Waumini wa  jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community wakiwa katika futari

Waumini wa dini ya kiislamu kwa upande wa wanawake wakiwa katika futari ya pamoja iliyofanyika jana jumapili Aug 28,2011 Silver Sring Maryland.

  
Washauri wa jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community Washngton DC Bwana Jabiri Jongo Picha ya kushoto Mh Uwesu Bakar wakiwa katika dua ya kisomo cha  kumuombea Marehemu Baba wa Dada yetu Jasmine Rubama, pamoja na kuwaombea jamaa zetu wote waliotangulia mbele. M/mungu awarehemu na awajaliee makazi meema peponi Amin.

Mh mgeni rashi Balozi Mwanaidi Maajar akiwa na waumini katika futari iliyoandaliwa na jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim  Community, kwenye ukumbi wa Hillandale Local Park, New Hampshire Avenue, Silver Spring Maryland Nchini Marekani.

Waumini wakipata futari ilioandaliwa na jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community Washngton DC

  
Dada zetu waliohudhuria katika futari ya pamoja kwenye ukumbi wa Hillandale  Local Park, mitaa ya  New Hampshire Avenue, Silver Spring Maryland.

Waumini wa dini ya kiislamu kwa upande wa wanawake wakipata flash ya pamoja baada ya kumaliza  futari  ya pamoja iliyoandaliwa na jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim  Community, katika ukumbi wa Hillandale  Local Park  New Hampshire Avenue, Silver Spring Maryland. Jana Jumapili Ramadhani ya 28, Aug 28,2011 picha zikiwa ni kama kumbukumbu ya Mwezi mtukufu wa ramadhani 2011 kutoka kwa mpiga picha wenu wa swahilivilla  Editor Abou Shatry.

Aunty yetu Saadie Fuad akipata flash ya pamoja na Amina Saleh katika futari ya pamoja


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community Washington Metropolitan (TAMCO) Mh. Iddi Sandaly akimkaribisha mgeni rasmi Mh Balozi Bi Mwanaidi Maajar


Mgeni rasmi katika futari ya pamoja akitoa hutuba fupi ya kuwa pongeza na kuwashukuru viongozi pamoja na wana Jumuiya ya kiislamu Tanzanian Muslim Community Washngton DC, na kutoa hutuba fupi ya kuhamasisha Watanzania waliokuwepo hapa Marekani kujumuika na  kusheherekea miaka 50 ya Uhuru wa Nchi yetu Tanzania. 

Angalia hutuba fupi iliotolewa na  Mh Balozi Mwanaidi Majaar Kwenye Futari  iliondaliwa na jumuiya ya Kiislamu Tanzanian Muslim Community Washngton DC.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA