TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Monday, August 29, 2011

FUTARI MJINI READING - UINGEREZA

2:32 PM

 
 Futari ilienda sambamba na kubadilishana mawazo
 Mh Naibu Balozi Chabaka akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa REACO
 Picha ya pamoja na wanajumuia
 Wanajumuia pamoja na wageni wakipata Futari kwa pamoja
Watoto wakipata futari
READING EASTERN AFRICAN COMMUNITY(REACO) Iliandaa futari maalum leo jioni 28.8.11 na kuwaalika wanajumuia mbalimbali kutoka Reading, London, Coventry na sehemu nyingine ili kupata futari kwa pamoja. Hii ni desturi ambayo hufanyika kila mwaka wakati huu wa mwezi mtukufu ramadhani. Lengu kuu haswa ni kujumuika pamoja katika kudumisha upendo, amani na umoja kwa wana jumuia pamoja,kuzingatia yale yote yalio mema na kukataza yalio Mabaya.

Mgeni Rasmi wa siku ya leo alikuwa Mh Naibu Balozi Chabaka Kilumanga alieambatana na baadhi ya maofisa wa ubalozi wetu wa Tanzania Hapa London.

Kwa niaba ya Mwenyekiti wa REACO Said Mahmud tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa wale wote walioitikia mwito na kuja kujiunga nasi. Tunawashuru sana.

Kwa maelezo au mawasiliano zaidi tafadhali tutumie email ifuatayo.reaco@hotmail.co.uk
Asanteni,

URBAN PULSE CREATIVE 

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA