TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Wednesday, July 21, 2010

Jeli ya kuzuia maambukizi ya HIV

11:50 AM

Watafiti wanasema jeli yenye dawa zinazopunguza makali ya ukimwi inayofanyiwa majaribio nchini Afrika kusini inaweza kupunguza kwa kiasi kikubwa uwezekano wa wanawake kuambukizwa virusi vya Ukimwi, inapotumiwa kila mara kabla ya tendo la ngono.

Shirika la afya duniani WHO na lile la kupambana na Ukimwi la Umoja wa Mataifa UNAIDS yametaja matokeo ya uchunguzi huo uliofanyiwa wanawake karibu 900 kama yenye mafanikio.

Jeli hiyo imetengenezwa hususan kukabili uambukizaji wa virusi vya Ukimwi, na imechanganywa na dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo ARVs.

Akizungumza katika mkutano huo wa Vienna, aliyekuwa rais wa Marekani Bill Clinton ametoa wito wa uwajibikaji zaidi na utumiaji bora wa fedha za kufadhili harakati dhidi ya kuenea virusi vya HIV.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA