TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Saturday, June 26, 2010

MWANAFUNZI WA SEKONDARI FRANK APANDA NGUZO ZA UMEME NIA KUTAKA KUWEPO KWA HAKI NCHINI

11:15 PM


Askari walipofanikiwa kumtoa FRANK juu ya nguzo hizo
FRANK akiwa juu ya NGUZO ya umeme maeneo ya UBUNGO
FRANK akiwa kwenye nguzo ya umeme askari wakiwa wanataka kumumtoa
Askari wakiwa katika harakati za kumuokoa.

Mwanafunzi wa kidato cha tatu katika shule ya KONA iliyoko MANZESE,DSM aliyejitambulisha kwa jina la FRANK hii leo amesababisha tafrani miongoni mwa wakazi wa jiji la DSM baada ya kukwea NGUZO ya umeme karibu na makutano ya Barabara za MANDELA na MOROGORO kwa madai ya kupinga kile alichokiita ukiukaji wa misingi ya utawala bora.
Ilikuwa majira ya saa nne asubuhi ambapo kijana FRANK aliparamia kazi ya fundi umeme na kukwea moja ya nguzo mpya za umeme iliyoko karibu na UBUNGO MATAA na kusababisha taharuki kwa wakazi wa maeneo hayo huku wengi wao wakisitisha shughuli za kawadida .

Baada ya muda askari wakafika na winchi kumtoa kijana huyo na kuelekea naye polisi kwa mahojiano zaidi.

Picha na MARTINA NGULUMBU WA TBC

1 comments:

Anonymous said...

Thats hw its started. I can see where we are going now. if u push people over a limit, they will have NOTHING TO LOSE. if you find a big group of oppressed like that, things will change in a real sense. not the nonsense which is going on now.

Post a Comment

 
BONYA HAPA