Ziara ya Mheshimiwa Dk. Kamala inatokana na ombi la wananchi hao kwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda alipotembelea London mwezi Mei mwaka huu. Mheshimmiwa Pinda aliwaahidi wananchi hao kumtuma Dk. Kamala kuja kutoa ufafanuzi kuhusiana na maendeleo na mapatano yaliyofikiwa katika Jumuiya hiyo.
Mmkutano huo ulifanyika katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania, London. Mikutano mengine miwili ya Waziri huyo na Watanzania itafanyika katika miji ya Reading leo Jumamosi, 19 Juni 2010 na Manchester ni kesho Jumapili, 20 Juni 2010, yote kuanzia saa kumi jioni.
Hotuba kamili ya Mheshimiwa Waziri itatangazwa kwenye tovuti ya Ubalozi baadae.
0 comments:
Post a Comment