


Wachezaji maarufu wa mchezo wa cricket nchini Australia watawasilisha orodha ya madai ya usalama kwa waandalizi wa maandalizi ya ligi kuu ya mchezo huo nchini India, kufuatia hofu yao kuhusu maandalizi ya ligi hiyo.
Timu ya Wachezaji hao maarufu bado haijaamua ikiwa watakwenda India kwa mechi kutokana na tisho la mashambulizi kutoka kwa makundi ya wanamgambo wenye ngome zao Pakistan.
Baada ya mkutano na wachezaji mjini Sydney, mkuu wa chama cha wachezaji wa Cricket Paul Marsh amesema, hofu imekuwa ikielezewa baada ya ripoti kutoka kwa mtaalam wa usalama ambayo ilielezea hofu kuhusu hali ya usalama nchini India.
0 comments:
Post a Comment