Kundi la Makhonya Royal Trust, ambalo lilitoa wazo hilo, lilielezea tambiko la kuchinja ng'ombe kuwa "njia muafaka ya kiafrika" kubariki mashindano hayo yatakayofanyika mwaka ujao.
Waziri katika serikali ya nchi hiyo, Sicelo Shiceka ameahidi kusaidia "kupigia debe" wazo hilo mbele ya shirikisho la soka la dunia, Fifa.
Lakini makundi ya haki za wanyama yametaka kushirikishwa kuombwa ushauri kuhusu mipango hiyo.
Mzozo huo umezeka wakati jaji mmoja wa Afrika Kusini alipokataa kuzuia karamu nyingine ya kabila la Zulu kuchinja dume la ng'ombe siku ya Jumamosi, badala yake alisema bunge la nchi hiyo linatakiwa kuamua.
0 comments:
Post a Comment