TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Wednesday, November 18, 2009

'Ole wenu wanahabari mnaovuruga amani'

10:02 PM
RAIS Jakaya Kikwete amerudia kuvionya vyombo vya habari nchini visitumie uhuru wao kuvuruga amani na kuvunja umoja wa kitaifa.

Rais Kikwete amesema, endapo vitafanya hivyo Serikali haiwezi kuviacha,vitashughilikiwa.

Sanjari na onyo hilo, Rais Kikwete amesema, Serikali itaendelea kulea na kudumisha uhuru wa vyombo vya habari.

Lakini Rais Kikwete amesema,vyombo vya habari lazima vijirekebishe,vitimize wajibu ambao ni sehemu muhimu ya uhuru huo wa habari.

“Kama nilivyowaambia pale Musoma majuzi wakati wa kuadhimisha miaka 10 ya kifo cha Mwalimu Nyerere, huu hauwezi kuwa uhuru wa kuvunja taifa, uhuru wa kugawa watu, uhuru wa kuchochea maasi na ugomvi kati ya dini mbalimbali, kati ya makabila, kati ya watu wenye rangi mbalimbali”

Alisema “Baadhi ya vyombo vyetu havina wajibu kabisa. Vinachochea maasi ya kuvunja nchi na kuleta mfarakano kati ya watu wetu. Vinajaribu kugawa watu wetu, kugawa mataifa yetu na kusababisha maafa makubwa. Hatuwezi kuvumilia vyombo vya habari vya namna hiyo vinavyotumia uhuru kuleta balaa kwa watu.”

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA