TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Friday, July 17, 2009

Kambi ya Guantanamo bay Wafungwa waibua sokomoko Guantanamo

2:12 PM
http://sanasaleem.files.wordpress.com/2008/11/060303_guantanamo_vmed_4pwidec2.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEic9MMohYbo-6nedi9sMikSzpD5FHxhxNGH7fljFlCDnONjOCQEEm27z7USX5UFSku2f5-EsYv3C7s8JW1FQw1Dhq-r6XZL4DiqpTAJ5RLTom5hmzAXB33bmMwhUpfvU_fD6OIXAFbjpuE/s400/guantanamo.jpg
Wafungwa watano, akiwemo anayedaiwa kupanga mashambulizi ya Septemba kumi na moja mjini New York, Halid Sheik Mohammed walikataa kufika mahakamani.

Hii ilitakiwa kuwa mara ya kwanza kwa washukukiwa hao kufika mahakamani tangu Barack Obama awe rais.

Ingawa Rais Obama amesimamisha kesi za washukiwa walioko Guantanamo bay bado zile za utangulizi zinaendelea.

Washukiwa hao wa ugaidi walitakiwa kuwepo mahakamani lakini Jaji alipofika viti vyao vilikuwa vitupu.

Jaji huyo hata hivyo alipinga pendekezo la mwendesha mashataka kuwa watolewe kutoka walipozuiliwa kwa nguvu.

Baada ya mahakama kuihairishwa kwa muda, washukiwa watatu walifika mbele ya jaji huyo.

Lakini mmoja wao, Mustafa al Hassawi aliomba kutoka mahakamani alipoambiwa kuwa hatapewa fursa ya kuzungumza.

Kesi hiyo ilitakiwa kubaini ikiwa Mustafa Al Hassawi na mwenzake Ramsey Bin Alsheeb wana akili timamu na uwezo wakujitetea.

Wakili wa Bin Alsheeb alielezea mahakama kuwa anatatizo la akili baada ya kuzuiwa kulala, lakini wakati alipokuwa anafafanua zaidi kipaza sauti cha mahakama kilizimwa.

Washukiwa hao walionyesha wazi kuwa wanadharau mahakama hiyo na hata mmoja alimchezea mwenzake kwa kumrushia mfano wa ndege aliotengeneza na karatasi bila kujali.


0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA