Na Hussein Semdoe, Handeni
MTOTO Hashiruna Hassan (5) ambaye ni mwanafunzi wa Shule ya Awali ya Suwa iliyopo katika Kijiji cha Suwa Kata ya Mazingara wilayani Handeni , amekufa baada ya kupigwa risasi na dada yake Mwanaidi Hassani (8).
Mwanaidi alimpiga Hashiruna risasi hiyo kichwani sehemu ya jicho kwa kutumia bunduki ya baba yao aina ya gobore wakati walipokuwa wakiichezea nyumbani kwao.
Akizungumzia suala hilo Afisa Mtendaji wa kata hiyo, Hassani Lugundi alisema tukio hilo lilitokea saa 4:00 usiku wa kuamikia jana.
Mgundi alisema wakati tukio hilo likitokea baba yao hakuwepo nyumbani kwake. Alisema kuwa tayari polisi wilaya ya Handeni walifika jana katika eneo la tukio.
0 comments:
Post a Comment