TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Thursday, August 15, 2013

WITO WA WANANCHI KWA BUNGE NA SERIKALI KUHUSU TOZO/ KODI YA LAINI YA SIMU

5:55 PM
Hivi karibuni bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilipitisha muswada wa sheria ya

fedha iliyosainiwa na rais Jakaya Kikwete na kuanza kutumika kama sheria kuanzia tarehe

01 August 2013. Sheria hii imetaja chanzo kimojawapo cha mapato kama tozo ya shilingi

1,000 kwa kila laini ya simu (sim card).

Kama mwitikio wa sheria hii, wananchi wengi kwenye mitandao ya kijamii waliipinga

tozo hii na kwa kupitia jukwaa la Change Tanzania, kuanzia tarehe 15 Julai 2013, juhudi

zilianza za kukusanya maoni ya wananchi kwa njia mbili: kwa njia ya mtandao – online

petition – na kwa njia ya kukusanya sahihi za wananchi mitaani.

Hadi kufikia tarehe 13 August 2013, Change Tanzania kwa njia hizi mbili imekusanya

zaidi ya sahihi elfu nne (4,000) kutoka mikoa mbalimbali ikiwemo Arusha, Dar es Salaam, 

Kigoma, Kilimanjaro, Morogoro, Manyara, Mwanza, Shinyanga, Singida, Songea, Zanzibar

na mikoa mingine. Juhudi bado zinaendelea za kukusanya sahihi zaidi.

Wito wa kusitisha tozo/kodi hii imeainisha kwa kina ni kwanini wananchi wanaipinga

ikiwa ni pamoja na kuwa kodi hii ya laini ya simu inamkandamiza mtanzania wa hali

ya kawaida na wa hali ya chini ambao ni 67% ya wananchi wanaoishi chini ya kipato

cha dola 1.25 (shs 2,000)  kwa siku. Takwimu zinaonyesha kuwa kati ya wamiliki wa

laini za simu milioni 22, milioni 8 wanatumia chini ya shilingi 1,000 kwa mwezi. Wito

huu umeeleza kuwa kuwaongezea mzigo wananchi hawa kwa kiwango ambacho tayari

wanashindwa kumudu ni kuwanyima kabisa fursa ya kutumia huduma hii muhimu.

Sababu nyingine iliyotajwa kwenye wito huu ni kuwa kodi hii haifuati misingi ya kulipa

kwa kadri ya matumizi na ni kodi kandamizi inayotozwa kwa wamiliki wa laini za simu

wote kwa kiasi kimoja bila kuzingatia kiwango cha matumizi. Wito huu unasisitiza kuwa

hii inamkandamiza mwananchi wa hali ya chini kwa kumlazimisha kulipa kiwango kikubwa

cha kodi ikiwa ni tofauti na mapato yake. Mfano uliotolewa kwenye wito huu ni wa mtu

anayetumia shilingi laki tano kwa mwezi kama muda wa maongezi na yule anayetumia

shilingi elfu tano - na tukilinganisha uwiano wa malipo haya na matumizi yao – basi

yule anayetumia shilingi laki tano analipa 0.2% ya matumizi yake, ila yule anayetumia

shilingi elfu tano anatozwa 20% ya matumizi yake. Aidha wito huu pia umeainisha

sababu nyingine ya kiuchumi kwani tayari kodi nyingi zimeongezwa kwenye sekta hii ya

mawasiliano. Wito huu umesisitiza kuwa kodi hii ni juu ya ongezeko la kodi mbalimbali

katika huduma za simu za mkononi ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa ushuru kutoka

12% kwenda 14.5% na pia kodi hii kutozwa kwa huduma zote ingawa awali ilitozwa

kwa huduma ya matumizi ya kuongea. Wito huu unainisha kuwa hivi sasa utumiaji wa

internet, kutuma na kupokea pesa kwa njia ya simu za mkononi unatozwa kodi, hivyo

ongezeko hili pekee limeshafanya huduma za simu za mkononi kupanda gharama kwa

kiasi kikubwa, na ongezeko la tozo/kodi ya shs 1,000 litazidi kuwaumiza wananchi.

Wito huu pia umependekeza kuwa mapato ya ndani yanaweza kupatikana kupitia njia

zingine mbadala ikiwa ni pamoja na serikali kupunguza matumizi yake mengineyo

(safari, posho, semina, manunuzi ya magari na kudhibiti ufisadi) na imetaja utafiti

uliofanywa na Interfaith Standing Committee on Economic Justice and the Integrity

of Creation mwaka jana uligundua kuwa kwa wastani Tanzania hupoteza dollar za

kimarekani billion moja (takriban shs trilioni 1.8) kila mwaka kutokana na ukwepaji kodi,

uhamishaji haramu wa fedha na misamaha ya kodi.

Sahihi hizi za wananchi ni fursa kwa mbunge au wabunge wataokuwa tayari kuitika wito

wa wananchi, wapiga kura wao na kupeleka hoja bungeni kwa ajili ya kufuta tozo/kodi hii,

tafadhali wawasiliane na CHANGE TANZANIA kwa namba zetu hapo chini. Pia unaweza

endelea kuweka sahihi yako kupitia mtandao huu hapa.

http://www.avaaz.org/en/petition/

WITO_WA_KUSITISHA_TOZOKODI_YA_LAINI_YA_SIMU_KILA_MWEZI_KUFUATIA_MABADILIKO_YA_SHERIA_YA_KODI_20

13/

Kuhusu Change Tanzania:

Change Tanzania ilianza mwaka 2012 kama mwamko wa wananchi waliopo katika

mtandao yaani social networks kwa maana ya Twitter na Facebook,  kutaka kujadili

masuala yanayohusu nchi yetu kama wananchi bila itikadi ya kisiasa na kwa kuzingatia

umuhimu wa kuwajibisha viongozi wa ngazi zote na hivyo kuleta mabadaliko chanya

katika jamii yetu kwa njia ya mijadala. Baada ya kupata wanachama zaidi ya elfu 20

(20,000) ndani ya mwezi moja, baadhi ya waanzilishi wa kikundi hiki cha mtandao

waliisajili kama kampuni isiyo na hisa yaani isiyotengeneza faida (not for profit

company). Leo hii ChangeTanzania ina wanachama zaidi ya elfu 30 Facebook, na wafuasi

zaidi ya elfu 6 (6,000) Twitter. Pia tuna blog na ukurasa wetu wa internet (website)

www.changetanzania.org.

Change Tanzania haipokei msaada wowote wa kifedha au udhamini kutoka mashirika

mengine, vyama au taasisi bali hutegemea michango ya wanachama wake tu.

Maria Sarungi Tsehai

MRATIBU

Simu: +255 783 034403

Barua pepe: sarungim@gmail.com

P.O. Box 105133, Dar es Salaam, TANZANIA

+255 22 2182405  |  +255 783 03 4403

info@changetanzania.org  |  www.changetanzania.org

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA