ADMISSIONS ARE NOW OFFICIALLY OPENED, CONTACT US FOR ENQUIRIES ON: SCHOLARSHIPS, UNIVERSITIES AND COURSES. APPLY NOW


Branches: ZANZIBAR, MWANZA, MOSHI, MOROCCO, MBEZI, TANGA, MASAKI, ARUSHA CITY, DAR-ES-SALAAM, DODOMA, ARUSHA MAIN, MAGOMENI, KARIAKOO, MBEYA, NYERERE ROAD, MBAGALA

Friday, July 31, 2009

Pinda ajitosa Waraka wa Kanisa Katoliki


Mjadala wa waraka wa Kanisa Katoliki ulioandaliwa kutoa elimu ya uraia kwa waumini wake kwa ajIli ya uchaguzi mkuu mwakani, umeibuka tena bungeni, hali iliyomfanya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuliomba kanisa kutopuuza maoni yanayotolewa juu yake.

Pinda alilazimika kutoa kauli hiyo jana wakati wa kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, kufuatia swali la Mbunge wa Chambani (CUF), Salim Hemed Khamis.

Khamis alitaka kujua msimamo wa serikali kuhusu waraka uliotolewa na kanisa hilo ambao hivi karibuni kumekuwa kukitolewa maoni mbalimbali na wanasiasa, wakiwemo wabunge, viongozi wa kidini na wananchi mbalimbali.

Pinda alisema sio mara ya kwanza kwa kanisa hilo kutoa waraka kama huo kwani walikwisha kufanya hivyo mara mbili huko nyuma, lakini hakukuwa na malalamiko kama ya safari hii.

“Sasa ninachoweza kusema mimi ni nini? Mimi si mara ya kwanza kuona ilani karibu kila wakati wa uchaguzi unapokaribia wamekuwa wakifanya hivyo. Lakini lazima tukubali vile vile kwamba mambo haya yanakwenda na wakati,” alisema. “Mara ya kwanza sikusikia maneno juu ya jambo hili yaani katika uchaguzi ule wa kwanza, lakini hata ule wa pili, lakini safari hii yamejitokeza,” alisema.

“Dhehebu hili ambalo wametoa jambo hili wasipuuze kauli za Watanzania zinazojitokeza sasa, na mimi nadhani kubwa hapa ni kwamba je, hivi kama kila dhehebu litaamua kutoa ilani yake tutakuwa na uwezo wa kudhibiti yale yaliyomo katika hizo ilani?” Alihoji na kuongeza: “Maana ndio wasiwasi wangu.”

“Kwa hiyo, upande wa serikali ni lazima vile vile waanze kufikiria kwamba pengine iko haja ya kuzungumza na madhehebu ya dini hata kama inabidi yatoe maelekezo fulani, pengine iko haja ya kusema hivi hamuwezi hayo mawazo yenu mkayaleta serikalini halafu yakatoka kwa mfumo mmoja kama yana nia nzuri ambayo hatuna uhakika kama yanasaidia kujenga umoja wa kitaifa au yanaweza yakapelekea kubomoka kwa umoja wa kitaifa,” alisema.

Alisema baada ya kusikiliza majadiliano marefu sana anadhani Wakatoliki wamesikia na akatoa rai kwamba wasipuuze kwani mengine ni majadiliano mazuri tu ya kujaribu kusema wanachohitaji watu.

“Sasa upande wa serikali tutaangalia tuone na sisi tunajipangaje na tufanye nini ili kuhakikisha umoja wa kitaifa unaendelea kuwepo maana ndiyo kazi kubwa tuliyonayo,” alisema.

Baada ya majibu hayo, Khamis aliuliza swali lingine la nyongeza, ambapo alianza na maelezo kwamba yanapotolewa matamko mazito kama haya ambayo yanagusa hisia za watu wengi, serikali inaonekana kuchelewa kuyatolea maelezo kama alivyofanya kwa ujasiri mkubwa Mbunge wa Kuteuliwa, Kingunge Ngombale Mwiru.

Ndipo akauliza: “Je, mheshimiwa Waziri Mkuu, huoni kama hii inakaribisha machafuko ya hali ya hewa kisiasa nchini wakati imechelewa na watu wanaendelea kubishana na kubishana?"

Katika majibu yake, Waziri Mkuu Pinda alisema: “Haraka haraka nayo haina baraka, wakati mwingine si vizuri ukaharakisha kuingilia kati wakati hujapata hasa tatizo likoje.”

Alisema yeye ana hakika kabisa kwamba baada ya mazungumzo marefu na mabishano ambayo yalikuwa yakiendelea, wako katika nafasi nzuri zaidi kama serikali kuona busara ipi sasa itumike katika kujaribu kuelekeza taifa na watu wake katika masuala kama haya.

“Kwa hiyo, mimi nadhani hatujakosea na wala sidhani tumefikia mahali ambapo nafikiri mchafuko wa hali ya hewa utajitokeza kwa sababu ya jambo hili, hapana. Mimi nadhani bado yako ndani ya uwezo wetu kuweza kulisimamia vizuri,” alisema Pinda

Mjadala kuhusu waraka ulioandaliwa na Kanisa Katoliki kwa ajili ya kuwapa waumini wake elimu ya uraia, uliibuka baada ya Kingunge kulitaka Kanisa hilo kuuondoa kwa maelezo kuwa unaweza kuwagawa Watanzania na kubomoa umoja wa kitaifa.

Kingunge alitoa madai hayo wakati akijadili hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo kwa mwaka 2009/10 iliyowasilishwa na waziri wa wizara hiyo, George Mkuchika.

Kutokana na kauli ya Kingunge, viongozi mbalimbali wa Katoliki nchini walimpuuza Kingunge na kumtaka aeleze sehemu yoyote ya waraka huo yenye matatizo kuliko kujikita katika kauli za kiujumla tu. Pia, baadhi walisema Kingunge alikuwa hajausoma waraka huo, huku watu wengine wakisema kwamba wanaoogopa waraka huo ni wakala wa mafisadi kwa kuwa unahimiza kuchaguliwa viongozi waadilifu.


Serikali yatoa kauli mkataba kati ya Tanzania na Canada


Serikali imetoa kauli yake kuhusu majadiliano ya mkataba wa Kukuza na Kulinda Vitega Uchumi kati ya Serikali ya Tanzania na ya Canada na kukanusha kwamba hauhusiani na suala la Tume ya Jaji Bomani iliyoundwa kushughulikia mapungufu katika sekta ya madini nchini.

Kauli hiyo ya Serikali ilitolewa jana bungeni na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo.

Hatua hiyo inafuatia swali la Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe alilomuuliza Waziri Mkuu Alhamisi ya wiki iliyopita, Julai 23, katika kipindi cha maswali ya papo kwa pao.

Kabwe alitaka kupata maelezo kutoka kwa Waziri Mkuu kwamba ni kwa nini taarifa ya Tume ya Jaji Bomani haijatungiwa sheria ili makampuni ya Canada na hasa katika sekta ya madini na mengineyo yaendelee kufaidika na utajiri uliopo nchini wa madini na kwamba Serikali ya Tanzania haijatoa taarifa kuhusu mkataba huo kwa umma ingawa majadiliano yanaendelea.

Akitoa kauli ya serikali, Mkulo alisema majadiliano ya mkataba wa kukuza na kulinda vitega uchumi kati ya Tanzania na Canada na Tume ya Jaji Bomani iliyoundwa kushughulikia mapungufu katika sekta ya madini nchini ni masuala mawili tofauti.

Alisema wakati Tume ya Jaji Bomani ilipewa jukumu la kudurusu mikataba na kuainisha mapungufu katika uwekezaji kwenye sekta ya madini, rasimu ya mkataba baina ya kukuza na kulinda vitega uchumi inaangalia masuala yanayohusu sekta zote za uwekezaji na kulinda vitega uchumi kwa jumla baina ya nchi zote mbili.

Alisema mchakato huo wa majadiliano baina ya nchi hizo mbili ulianza mwanzoni mwa mwaka 2004 na kufuatiwa na majadiliano yasiyo rasmi ya Novemba 5 na 6 mwaka 2007 ambapo awamu ya kwanza yalifanyika Ottawa nchini Canada mwaka 2008 na kufuatiwa na ya tatu ya Septemba 15 hadi 19 mwaka huo huo wa 2008.

Mkulo alifafanua kuwa hadi kumalizika kwa majadiliano ya tatu, pande zote mbili bado hazijakubaliana kwenye vipengele vingi vya rasimu ya mkataba na hivi sasa kamati ya majadiliano inapitia mapendekezo mapya yaliwasilishwa na Serikali ya Canada kuhusu rasimu ya mkataba husika kabla ya kuanza tena majadiliano ya awamu ya nne.

Alibainisha kuwa chimbuko la majadiliano hayo ni baada ya Tanzania kuridhia mikataba iliyoanzishwa na ‘Multilateral Investment Guarantee Agency (MIGA)’ pamoja na ile ya ‘International Centre for Settlement of Investment Disputes (ICSID)’ kuwa migogoro inayotokana na vitega uchumi vilivyoelekezwa na wawekezaji iwe inasuluhishwa kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na kukubaliwa kimataifa.

Mkulo alivitaja vipengele muhimu vinavyozingatiwa katika makubaliano na nchi mbalimbali kuhusu mikataba hiyo kwamba ni pamoja na uendelezaji wa uwekezaji rasilimali, ulinzi wa vitega uchumi, utoaji wa vivutio kwa wawekezaji, utaifishaji wa rasilimali, fidia wakati wa matukio yasiyokuwa ya kawaida kama vile vita na machafuko.

Vipengele vingine alisema ni pamoja na uhamasishaji mali na faida, usuluhishi wa migogoro na utaratibu wa muda wa kuanza utekelezaji wa makubaliano.

Kwa mujibu wa Waziri, lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa maslahi ya Taifa yanalindwa na pia mikataba hiyo inalenga kuwajengea imani na uhakika wawekezaji kutoka nje kwamba vitega uchumi vyao vitakuwa salama nchini Tanzania kama sera ya kukuza uwekezaji ya mwaka 1996 inavyoelekeza.

Tanzania ina mikataba ya aina hiyo na kwamba tayari inatekelezwa baina ya nchi za Uingereza, Sweden, Denmark, Finland, Italia, Uholanzi, Uswisi, Afrika ya Kusini na Mauritius

Upinzani washangaa kuona Epa bado inatema pesa


Kambi ya upinzani bungeni imesema imeingiwa na wasiwasi kuhusu hatua ya serikali kutoa dhamana kwa ajili ya malipo kupitia Akaunti ya Madeni ya Nje (Epa) katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ya shilingi bilioni 65 katika kipindi hiki kinachokaribia uchaguzi mkuu.

Akizungumza kwa niaba ya kiongozi wa kambi hiyo, Hamad Rashid Mohammed, Mbunge wa Viti Maalum, Fatma Fereji, alisema katika taarifa ya mwaka ya BoT ya 2007/2008 ambayo iliwasilishwa bungeni, imeonekana kuwa serikali ilitoa dhamana ya Epa ya sh. bilioni 65.

Alisema wakati Rais alipohutubia Bunge mwaka 2008 alisema malipo ya Epa yamesimama, lakini serikali bado imetoa ‘special Epa stock’ yenye thamani ya fedha hizo.

“Mara kwa mara serikali imekuwa ikirudia kusema kuwa malipo ya Epa yamefungwa, vile vile Benki Kuu kupitia kamati mbalimbali za Bunge imesema hivyo hivyo, kumbe hali ni tofauti,” alishangaa.

Alisema kambi ya upinzani inapata mashaka zaidi kwamba malipo haya mapya ya Epa yanafanyika kipindi kinachokaribia uchaguzi mkuu 2010 kwa lengo la kukinufaisha chama tawala kisiasa.

Alisema katika mazingira ya sasa ambapo nchi haina sheria ya kudhibiti matumizi ya fedha katika kampeni, na kwamba Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Fedha za Serikali (CAG), hajaanza kukagua vyama vya siasa ili kujua vyanzo vya mapato, ni dhahiri Epa hii maalum ni kiwingu na kwamba kambi ya upinzani inahitaji kupata maelezo ya kinachohusu ‘special Epa stock.’

Akizungumzia azma ya serikali ya kuanzisha upya Mpango wa Kuondoa na Kukuza Uchumi Tanzania (Mkukuta), kambi ya upinzani imeshauri kuwa Mkukuta mpya usianzishwe ili kuondoa mashaka kuwa moja ya chama cha siasa kinatumia Mkukuta kama ilani yake ya uchaguzi na hivyo kuzuia mawazo huru yenye kuweza kuchangia dira ya taifa baada ya mchakato wa uchaguzi mkuu wa mwakani.

Kambi hiyo ilishauri kuwa Mkukuta mpya uanze mwaka 2011 na upitishwe na Bunge la Kumi.

Kuhusu mradi mkubwa wa vitambulisho vya taifa, kambi hiyo ilisema imefanya utafiti na kugundua kuwa gharama zinazozungumziwa ni kubwa mno, bila ya sababu, kwani vitambulisho vya aina hii vimewahi kutengenezwa Uholanzi, Afrika Kusini, Nepal na Peru, lakini hata ndani ya nchi, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetengeneza vitambulisho 500,000 kwa gharama ya dola za Marekani milioni 3 tu.


Obama, Crowley and Gates chat over beers

US President Barack Obama (R) sits alongside Police Sergeant James Crowley (2nd R) of Cambridge, Massachusetts, and Harvard Professor Henry Louis Gates Jr. (2nd L), alongside US Vice President Joe Biden (L) as they share beers on the South Lawn near the Oval Office at the White House in Washington, DC.

Spika Sitta aomba ulinzi zaidi, adai nguvu ya mafisadi inahatarisha maisha yake

Spika Sitta aomba ulinzi zaidi, adai nguvu ya mafisadi inahatarisha maisha yake

Kizitto Noya, Dodoma na Boniface Meena

SPIKA wa Bunge Samuel Sitta ameiomba Serikali kumwongezea ulinzi kwa kuwa mafisadi wameongeza nguvu ya vita dhidi yake.

Spika Sitta alisema hayo alipokuwa akizungumzia tuhuma dhidi yake, zilizoripotiwa jana na baadhi ya vyombo vya habari (sio Mwananchi) kuwa anafanya njama kuchoma nyaraka za Bunge.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, Spika anadaiwa kula njama ili kuchoma ofisi ya mhasibu wa Bunge ili kuharibu nyaraka muhimu zinazomhusisha na ubadhirifu wa fedha za Bunge.

Lakini Spika Sitta alijibu tuhuma hizo bungeni akisema taarifa hizo zina mkono wa wabaya wake, wenye lengo la kumchafua katika utendaji wake.

“Hivi kama kweli nataka kuficha faili la Bunge nani anaweza kunizuia humu ndani?” alihoji Spika Sitta na kuongeza:

“Hizi ni taarifa za wabaya wangu, wanachofanya ni kuziweka kwenye internet kwanza halafu wanazisambaza kwenye vyombo vyao maalum, magazeti manne; gazeti la Tazama, Tanzania Daima na mengine mnayoyaona," alisema Spika na kuongeza:

“Mheshimiwa Waziri Mkuu naomba mnipe ulinzi zaidi, hii vita ni ngumu na kubwa sasa. Ulinzi mnaonipa naona hautoshi,” alilalamika Spika Sitta na kuwaponda wanaomwandama kuwa hata iweje, ataendelea kushinda ubunge jimboni kwake na kuwa Spika kama bado atakuwa hai mwakani.

Alifafanua kuwa fedha wanazopeleka maadui zake jimboni kwake Urambo zinasaidia kuimarisha maendeleo, lakini hazitomng’oa madarakani.

"Wananchi wangu wanajua ninachokifanya jimboni kwangu, hata wakipeleka pikipiki bado nitashinda," alisema Sitta.

Mara kwa mara Spika Sitta amekuwa akidai kwamba anaandamwa na mafisadi ambao wanataka aache kufichua maovu yao.

Spika Sitta alisema hayo muda mfupi baada ya kumaliza kutoa mwongozo kwa mbunge wa Micheweni (CUF), Shoka Khamis Juma, kwamba chama fulani kina tabia ya kununua shahada za kura wakati wa chaguzi.

Katika mwongozo wake, Spika alimtaka mbunge huyo kufuta kauli yake bungeni kwa kuwa ushahidi aliotoa kuthibitisha kauli hiyo ni dhaifu.

“Madai ya Shoka ni tuhuma kama tuhuma zozote zinazotolewa na wanasiasa wengine,” alisema.

Akifafanua kuwa Shoka ameshindwa kuthibitisha tuhuma zake kwa kuwa ametoa ushahidi wa magazeti ambayo sio yote yanaweza kuaminika.

“Magazeti yanaweza kuwa chanzo cha taarifa kwa wabunge katika kuchangia hoja zao, lakini sio kigezo pekee cha kumwezesha Spika kutoa mwongozo,” alisema Sitta na kuendelea:

“Hivyo mheshimiwa Shoka hawezi kulindwa na kifungu namba 63 (2), kwa mantiki hiyo namtaka kwa kanuni namba 63 (1) afute kauli yake humu bungeni kabla ya kumalizika kikao hiki cha Bunge”.

Juni 12 mwaka huu mbunge huyo wa CUF alitamka bungeni alipokuwa akiuliza swali la nyongeza kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimekuwa na tabia ya kuiba shahada za kupigia katika maeneo ambayo kinaona hakiungwi mkono.

Naibu Spika Anne Makinda ambaye alikuwa anaongoza kikao cha Bunge siku hiyo, alimtaka mbunge huyo athibitishe kauli yake, naye alifanya hivyo Juni 17, mwaka huu kwa kuwasilisha kwa Spika nakala za magazeti yaliyoripoti uchaguzi wa Jimbo la Busanda.

Hata hivyo, Spika Sitta alisema kwa kuwa hakuna ushahidi wa hukumu kuhusu tuhuma hizo, madai ya Shoka ni tuhuma kama tuhuma zingine zinazotolewa na wanasiasa majukwaani, hivyo kumtaka afute madai yake.




IJUMAA SHOWBIZ!

kanumba
france
femi
mercy
Kanumba kuingiza kitaani The Director na Wanigeria
Msanii maarufu wa filamu nchini, Steven Kanumba anatarajia kutoa filamu mpya inayokwenda kwa jina la The director ambayo inaelezwa kuwa itakuwa ni moto wa kuotea mbali.

Kanumba ameitonya safu hii kuwa, katika filamu hiyo ya Kiswahili itakayofichua kinachofanywa nyuma ya pazia wakati wa kurekodi filamu za kibongo, amewashirikisha wasanii wakali kutoka Nigeria ambao ni Nkiru Sylvanus, Mercy Johnson ‘Ble Ble’, Emmanuel Francis na Femi Ogdebe.

Mbali na wanaijeria hao pia yumo Elizabeth Chijumba ‘Nikita’, Halfan Ahmed ‘Kevin’ na Suzan Lewis ‘Natasha’.

“Kwa kweli itakuwa ni filamu ya aina yake ambayo huenda ikafunika zote nilizowahi kuzitoa na naamini mashabiki wangu wataifurahia,”alisema Kanumba.
Kwa mujibu wa Kanumba, Filamu hiyo imeandaliwa chini ya Kampuni ya The Game 1st Quality itakuwa mtaani siku chache zijazo.

Wakati huo huo, Kanumba anasubiriwa katika mazoezi ya filamu ya Tears on Valentines inayoandaliwa chini ya Kampuni ya Tollywood Movies yaliyoanza mwanzoni mwa wiki hii jijini Dar es Salaam.


Thursday, July 30, 2009

Mkutano wa kuanzisha jumuia ya watanzania katika Jimbo la Gauteng
Watanzania waishio katika Jimbo la Gauteng (Johannesburg na Pretoria) wanatarajia kufanya mkutano wa kuanzisha jumuia yao tarehe 22 mwezi wa Agosti 2009 jijini Johannesburg.
Mkutano huu utatoa fursa ya kujadili mambo mbali mbali yatakayohusu jumuia hii pamoja na kuchagua viongozi wa kudumu.


Watanzania wanaoishi kwenye miji ya Johannesburg na Pretoria ambao wangependa kuwa wanachama na pia kushiriki kwenye uchaguzi wa uongozi wa jumuia wanakaribishwa kuwasiliana na wajumbe wafuatao kwa maelezo zaidi:
  1. Brian Mshana b_mshana@yahoo.com
  2. Laurean Rugambwa bwanakunu@gmail.com
  3. Faustine Ndugulile drfaustinen@aol.com

Shukrani
KAMATI YA MAANDALIZI

Nigeria; wanajeshi waushambulia msikiti


Vikosi vya Nigeria vimeushambulia msikiti mmoja ambako wapiganaji wa kundi moja la Kiislamu linalolaumiwa kwa kuzusha ghasia limekuwa likijificha.

Taarifa zinaelezea kwamba wapiganaji wengi wameuawa katika mapigano hayo, ambayo yamefanyika siku ya tatu tangu ghasia kuzuka katika mji wa kaskazini wa Maiduguri.

Wengi ya wapiganaji hao sasa wametoroka, huku wakivishambulia vituo kadha vya polisi.

Kundi hilo la wapiganaji la Kiislamu, linalofahamika kama Boko Haram, linataka kuipindua serikali, na kuanzisha mfumo wa sharia za Kiislamu katika kuiongoza nchi.

Vikosi viliushambulia msikiti huo, baada ya wanajeshi 1,000 zaidi kupelekwa katika mji huo.

Kamanda wa wanajeshi wa nchi kavu, Meja Jenerali Saleh Maina, aliliambia shirika la habari la Associated Press kwamba naibu wa kiongozi wa kundi hilo, aliuawa katika mapigano hayo, usiku wa Jumatano.

MAMA PINDA

Mke wa Waziri Mkuu, Tunu Pinda akizungumza na mtoto Amani baada ya kuwasili kwenye kituo kinacholea watoto yatima cha Nyumba ya Matumaini cha Miyuji, Dodoma.

Wateja kulipia ankra za maji kupitia mtandao wa simu Vodafone M-PESA

Na Zaina Malongo

KATIKA kuhakikisha kwamba maisha ya Watanzania yanaboreshwa, Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na kampuni ya usambazaji wa maji jijini, Dawasco, imeanzisha huduma ya bure kulipia ankara zao kwa kupitia huduma ya Vodafone M-PESA.

Akizungumza hivi karibuni Makao Makuu ya Dawasco wakati wa hafla ya makubaliano ya kutoa huduma hiyo, Mkurugenzi wa Masoko wa Vodacom Tanzania Ephraim Mafuru alisema huduma hiyo ni ubunifu mwingine wa Vodacom unaolenga kuboresha maisha ya wateja wake.

Alisema kupitia huduma hiyo, wateja wa Vodacom Tanzania, wanaweza kulipa ankara zao za maji viganjani mwao kwa kutumia simu zao za mkononi badala ya kupanga foleni ndefu kwa lengo la kulipa ankara zao.

“Haya mapinduzi makubwa yanayoletwa na Vodacom Tanzania, mtandao unaoongoza hapa nchini, wateja wetu wategemee makubwa zaidi,” alisema Mafuru.

Alisema Vodacom Tanzania inapenda kuwakaribisha DAWASCO katika ulimwengu wa Vodafone M-Pesa na kwamba, anafarijika kuona kwamba wadau mbalimbali wanashirikiana na Vodacom kufanikisha huduma mbalimbali kwa umma.

Mwaka jana mwezi Aprili, Vodacom Tanzania, ilizindua rasmi huduma yake ya kutuma pesa kwa kutumia simu za mkononi ijulikanayo kama Vodafone M-Pesa. Huduma inayotolewa na mtandao wa Vodacom kwa kushirikiana na kundi la Vodafone.

Waziri wa Fedha na Uchumi Mustafa Mkulo, ndiye aliyeizindua rasmi huduma hiyo na aliipongeza Vodacom kwa kuanzisha huduma hiyo muhimu hapa nchini.

Naye Afisa Biashara wa Dawasco, Raymond Mndolwa, aliipongeza Vodacom kwa ushirikiano huo ambao pia unalenga katika kuboresha huduma za Dawasco.

Kumbuka mitandao ya Vodacom inapatikana ndani na nje ya nchi yetu, kwa hiyo haijalishi kama uko hapa Tanzania au nje ya nchi, bado unaweza kulipia ankara yako popote na Vodafone M-Pesa.



JWTZ lamkana askari wake aliyekamatwa kwa ujambazi


Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limemkana askari wake, koplo Julius Abraham Kwayu, ambaye alidaiwa kuhusika katika tukio la ujambazi lililotokea Julai 24 mwaka huu, Manzese jijini Dar es Salaam na kueleza kwamba aliomba likizo na hakurejea kwa muda mrefu.

Taarifa ya JWTZ iliyotolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano makao makuu ya Jeshi hilo kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana ilisema Koplo Kwayu, alikuwa mtoro wa jeshi kwa kipindi kirefu na kwamba jeshi lilikuwa likimtafuta.

JWTZ katika taarifa hiyo, limempongeza Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova na kikosi chake kwa kufanikisha kuwatia mbaroni majambazi hao.

"JWTZ, Polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama wanashirikiana kwa karibu kufuatilia mwenendo wa watumishi wasiokuwa waaminifu kama ilivyojitokeza kwa Koplo Julius Abraham katika matukio mengine kama hayo ya ujambazi," ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Hata hivyo, taarifa hiyo ilifafanua kuwa ili kukabiliana na tabia mbaya kwa baadhi ya watumishi, jeshi limebadili utaratibu wa kuajiri askari wapya na kwamba kuanzia sasa vijana wote wanaoomba kujiunga na JWTZ watalazimika kupata mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) au Jeshi la kujenga Uchumi (JKU) ili wachunguzwe mienendo yao.


Mabilioni ya JK wamekula wakurugenzi, wabunge`


Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wamesema fedha zilizotolewa na serikali ili kusaidia wazalishaji wadogo wadogo, maarufu kama mamilioni ya JK, hazijawanufaisha masikini visiwani hapa kwa sababu wamekopeshwa wabunge na wakurugenzi.

Wawakilishi hao, waliyasema hayo wakati wakichangia Bajeti ya Wizara ya Kazi, Maendeleo ya Vijana, Wanawake na Watoto kwa mwaka wa fedha 2009/10 katika kikao chao kinachoendelea mjini Unguja.

Mwakilishi wa jimbo la Kiwani, Hija Hassan Hija, alisema ana ushahidi wa fedha hizo kukopeshwa wabunge na Wakurugenzi na siyo walengwa kama ilivyokusudiwa na Rais Jakaya Kikwete.

Alisema wananchi waliopaswa kunufaika na fedha hizo wamekuwa wakitumia muda mwingi kuzifuatilia, lakini wengi hawajanufaika nazo.

Alisema kitendo hicho ni kinyume na misingi ya utawala bora na hivyo akaitaka serikali kuchukua hatua stahili ili walengwa wazipate.

Nae Mwakilishi wa Viti Maalum, Zakia Omar Juma alisema kwamba mifuko ya maendeleo inayoanzishwa na viongozi, lazima ilenge kuwainua akinamama wanaoishi katika mazingira magumu ya kimaisha.

Hata hivyo, aliitaka serikali itoe maelezo akinamama wa Zanzibar wamekuwa wakinufaika vipi na mfuko wa maendeleo ya wanawake ulioanzishwa na mke wa Rais, Mama Salma Kikwete na ule ulioanzishwa na Jumuiya ya Zayedesa, inayoongozwa na mke wa Rais Karume, Mama Shadya.

Alisema kwamba kuna akinamama wengi wanaishi katika mazingira magumu ya umasikini hasa katika Wilaya ya Micheweni Pemba, lakini hawaonekani kulengwa kuinuliwa kiuchumi na mifuko hiyo.

Mwakilishi wa Viti Maalum, Najma Khalfan alisema tatizo la vijana kuijiingiza katika vitendo vya ukahaba vinatokana na msukumo mdogo wa serikali katika kuwawezesha kupata ajira.


laurence masha mgeni rasmi miss redds kinondoni 2009

Baadhi ya walimbwende wa redds miss kinondoni 2009 ndani ya mjengoni jioni hii
Moja ya kichwa mahiri kupitia fani ya utangazaji ndani ya Clouds Fm 88.4 alias Mjengoni Kapt Gadner G Habash akizungumza na walimbwende watakaoshiriki kuwania taji la Redds Miss Kinondoni 2009 leo jioni mjengoni hapo Mikocheni,jijini Dar kuhusiana na namna walivyojiandaa kwenye mchuano huo mkali na wa kuvutia.
Aidha shindano hilo lililoandaliwa na kampuni ya Boy George Promotions limeweka bayana zawadi mbalimbali watakazozinyakuwa washiriki hao,ambapo mshindi wa kwanza ataibuka na kitita cha shilingi milioni moja na laki tano taslim,mshindi wa pili atanyakua kitita cha shilingi milioni Moja,mshindi wa tatu atapata shilingi Laki nane,mshindi wa nne na tano watajinyakulia kiasi cha shilingi laki tatu kila mmoja na waliobaki watapata kifuta jasho cha shilingi laki moja na nusu.
Onesho hilo litakalofanyika siku ya ijumaa pale Mlimani City-Mwenge jijini Dar,kiingilio kimepangwa kuwa ni 10,000 kwa viti vya kawaida na viti maalumu kwa shilingi 40,000/= kwa kila kichwa.Kwa upande wa burudani kundi la Wazee wa Ngwasuma litatoa burudani kambambe kwa wegeni mbalimbali watakaofika katika onesho hilo.
Katika onesho hilo mgeni rasmi atakuw ni Waziri wa mambo ya Ndani Mh.Laurence Masha

Wednesday, July 29, 2009

kipanya

Kiwanda cha Bia (TBL) chaungua moto

tutakunywa juice? TANZANIA BREWERIES YAUNGUA MOTO

Usiku wa kuamkia leo kiwanda cha bia TBL kimewaka moto upande wa crates tupu, ni moto mkubwa sana, hadi sasa haijajulikana hasara iliyopatikana.hawa watu wapo makini sana na majanga sasa hili sijui ni nani ataevishwa shanga!! chanzo insider

Marekani yalipa suala la makazi kipaumbele


Mjumbe wa Marekani kuhusu amani ya Mashariki ya Kati George Mitchell ametoa wito kwa pande zote husika kufanya maamuzi mazito kwa manufaa ya amani ya Mashariki ya Kati.

Mjumbe Mitchell and waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema walikuwa na mazungumzo yaliokuwa na mtazamo mzuri unaonuia kuanzisha tena utaratibu wa amani wa Mashariki ya Kati.

Suala la Israel kusimamisha ujenzi wake katika maeneo ya Wapalestina halikutajwa japo Marekani imekuwa inadai ujenzi huo usitishwe mara moja.

Bw. Mitchell ni mmoja wa maafisa wakuu wa Marekani katika eneo hilo wanaojaribu kushughulikia mpango wa amani wa Mashariki ya Kati.
Wapalestina kwa upande wao wamesema ujenzi wote wa Israel katika maeneo yaliokaliwa kimabavu lazima ukomeshwe kabla ya mazungumzo kuanza.

Uhusiano mbaya

Baada ya mkutano uliochukuwa karibu saa tatu uliotarajiwa kuangazia zaidi suala la makazi, mabwana hao wawili walizungumza na waandishi wa habari kwa kifupi. Suala la Ujenzi halikutajwa kamwe.

Bw. Netanyahu alisema wanapiga hatua kuh usu kuafikia maelewano yatakayo wawezesha kuendelea na kukamilisha utaratibu wa amani kati ya majirani wa Palestina na nchi nyengine katika eneo hilo .

Uhusiano kati ya maswahiba hawa wawili ulionekana kutikisika kidogo katika wiki za hivi karibuni baada ya Marekani kudai ujenzi unaofanywa na Israel katika maeneo yanayokaliwa kimabavu ukomeshwe mara moja.

Marekani inatilia mkazo hatua za kidiplomasia katika kuafikia mpango madhubuti wa amani ya Mashariki ya Kati. Mshauri wa kitaifa wa Rais Barack Obama James Jones na mwanadiplomasia Dennis Ross pia wanatarajiwa kuwasili katika eneo hilo kuchangia katika juhudi hizo za kuleta amani.

Awali, mjumbe Mitchell alimwambia Rais wa Israel Shimon Peres kwamba Israel inaweza kuimarisha hali ilivyo sasa kwa kukabiliana na masuala nyeti kama vile ujenzi wa makazi ya Israel katika maeneo yaliokaliwa na vile vile vituo vya ukaguzi kuingia na kutoka maeneo ya wapalestina.


Tuesday, July 28, 2009

Taylor akana kula nyama ya binadamu


"Huo ni upuzi mtupu", alihamaki kiongozi wa zamani wa Liberia, Charles Taylor kuhusu madai kwamba aliwahi kula nyama ya binadamu na kuwaamuru wanamgambo wake kuwala mahasimu wake.

Baadhi ya wapiganaji wa Bwana Taylor walidai mbele ya mahakama The Hague inayosikiliza kesi hiyo kwamba walilalizimishwa na kiongozi huyo wa zamani kula miili ya maadui wake.

Lakini Bwana Taylor mwenye umri wa miaka 61 alikemea madai hayo kama upuzi mtupu akisema, "yananikera, na inaudhi ikiwa unayaamini madai kama hayo."

Rais huyo wa zamani ndiye kiongozi wa kwanza kufikishwa mbele ya mahakama ya kimataifa.

Amekanusha madai mengine 11 yanayohusiana na vita vya wenyewe kwa wenyewe katika nchi jirani ya Sierra Leone.

Inadaiwa kwamba Bwana Taylor aliwapa silaha na maagizo waasi katika nchi yake ya Liberia kuvamia Sierra Leone na kupora rasilmali zake za almasi.

Miongoni wa madai yanayomkabili ni ugaidi, mauaji, ubakaji na dhuluma.

Alipoanza kujitetea wiki tatu zilizopita, Bwana Taylor alisema ingekuwa vigumu kuendesha biashara ya silaha na madini ya almasi kutoka Sierra Leone kwa sababu ya hali mbovu ya barabara nchini humo.

Alisema madai ya kumla binadamu, yanamfanya "kuhisi kichefuchefu".

Bwana Taylor alisema

Shahidi mmoja alikuwa ameiambia mahakama kwamba aliamrishwa na Bwana Taylor kula nyama ya binadamu.

Lakini rais huyo wa zamani alitupuuzilia mbali madai hayo akisema, "sikuwahi kutoa amri kama hiyo. Jambo hilo halikufanyika."

Liyumba: Mambo magumu!


Mambo yameendelea kuwa magumu katika kesi inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala wa Benki Kuu ya Tanzania, BoT, Amatus Liyumba baada ya jaribio la mawakili wa mshtakiwa huyo waliotaka kesi hiyo ifutwe kugonga mwamba leo asubuhi.

Badala yake, kesi hiyo sasa itaanza kuunguruma mbele ya jopo la mahakimu watatu kuanzia Agosti 11, mwaka huu.

Aliyetoa uamuzi huo ni Hakimu Mkazi Eva Nkya, ikia ni baada ya kusikiliza pande mbili za kesi hiyo zilizokuwa zikilumbana vikali mahakamani hapo leo asubuhi.

Upande wa utetezi uliokuwa chini ya wakili Majura Magafu ulitoa hoja ya kutaka kesi hiyo ifutwe kwa sababu siku 60 zinazotakiwa kwa mujibu wa sheria zimepita bila ya upelelezi kukamilika.

Hata hivyo, upande wa Jamhuri uliokuwa chini ya Wakili wa Serikali Justine Mulokozi, ulidai kuwa ulikuwa ukifuata taratibu na kwamba sasa, upelelezi wa kesi hiyo umekamilika.

Baada ya kueleza hivyo (kuwa upelelezi umekamilika), wakili Mulokozi akaiomba mahakama kupanga tarehe ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo.

Akitoa uamuzi wake, Hakimu Nkya akasema amesikiliza hoja za pande zote mbili na kwamba kutokana na uzito wa kesi hiyo, itabidi isikilizwe mbele ya jopo la mahakimu watatu.

Baada ya hapo, akaiahirisha kesi hiyo hadi Agosti 11 mwaka huu ambapo mshtakiwa anatarajiwa kusomewa maelezo ya awali.

Liyumba ambaye amerudishwa rumande hadi siku hiyo (Agosti 11), anakabiliwa na kesi ya kutumia vibaya madaraka yake na kuisababishia Serikali hasara ya zaidi shilingi bilioni 221, katika mradi wa majengo pacha ya benki kuu (BoT).


Mafua ya nguruwe yarejea Dar wazungu wawili wagundulika uwanja wa ndege

Hussein Issa na Glory Kimath

WIKI tatu baada ya mgonjwa wa kwanza wa homa ya mafua ya nguruwe raia wa Uingereza kugundulika Dar es Salama, wagonjwa wengine wawili raia wa nchi hiyo wamegundulika kuwa nao na kukimbizwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa matibabu.

Raia hao ambao ni ndugu wa familia moja, wanaoishi Mbezi Beach jijini, walibainika kuwa na ugonjwa huo Jumapili iliyopita katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere wakati wakirejea kutoka Nairobi, Kenya walikokwenda kukutana na ndugu zao.

Baada ya kubainika kuwa na ugonjwa huo walipelekwa moja kwa moja Muhimbili ambako wamelazwa kwa ajili ya matibabu.

Mgonjwa wa kwanza hapa nchini aligundulika Julai 4, mwaka huu katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere wakati akiingia nchini kwa ndege ya Shirika la Ndege la Kenya.

Taarifa ya Wizara ya Afya ilisema raia huyo wa Uingereza alitoka London na kutua Nairobi, Kenya kabla ya kuingia nchini.

Mkurugenzi wa Huduma ya Tiba wa MNH, Profesa Andrew Swai alithibitisha jana kuwepo kwa wagonjwa hao katika hospitali hiyo, lakini alikataa kutaja majina yao kwa maelezo kwamba, kufanya hivyo ni kinyume cha maadili ya kazi yao.

"Hawa kina dada ambao nadhani ni ndugu ni raia wa Uingereza, walitokea Kenya katika mkutano na ndugu zao wanaoishi huko; ila sio vizuri kuwataja majina kwani kisheria tukiwataja ni kuwadhalilisha na wakitoka watu watawasumbua," alisema Profesa Swai.

Aliongeza kuwa majina yao hayana faida kwa jamii, ila kinachotakiwa ni kufahamika kuwa ugonjwa huo upo na wananchi wawe makini sana, hususan wanaokwenda nje ya nchi na wanaoishi mpakani, ili wasipate maambukizo.

Profesa Swai, alisema wagonjwa hao waliletwa siku ya Julai 26 mwaka huu hospitalini Muhimbili wakitokea uwanja wa ndege wa kimataifa, Julius Nyerere.

"Unajua tumejizatiti kukabiliana na ugonjwa huo kila kona, kuanzia katika mipaka ya kuingia nchini, bandarini na viwanja vya ndege vilivyopo nchini; hivyo ilikuwa rahisi kuwatambua wagonjwa hao," alisema Profesa Swai.

Hata hivyo alifahamisha kuwa wagonjwa hao wanaendelea vizuri na matibabu na kwamba, muda wowote wanaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani kwao.

Gazeti hili lilipata taarifa za kuwepo kwa wagonjwa hao tangu juzi na lilipofika Muhimbili kupata ukweli na ufafanuzi wake, maafisa uhusiano wa Muhimbili hawakusema lolote.

Chanzo cha taarifa hizo kililiambia gazeti hili kuwa wagonjwa hao ambao ni ndugu walipelekwa hospitalini hapo kwa gari la wagonjwa la Uwanja wa ndege wa Julius Nyerere juzi majira ya saa kumi jioni.

Kilifahamisha kuwa wagonjwa hao wamelazwa katika chumba maalumu katika hospitali hiyo, kinachojulikana na baadhi ya wauguzi, ili habari za kuwepo kwa wagonjwa hao nchini zisienee kwa wananchi na hatimaye kuwatia hofu.

“Unaona wamelazwa katika vyumba vile, lakini hutakiwi kusogea pale kwani watakushangaa wewe ni nani na pia usalama wako kiafya utakuwa hatarini, kuambukizwa ugonjwa huo,” kilisema chanzo chetu hospitalini hapo na kuongeza:

“Viongozi wa hospitali wanafanya siri, hata sisi na wauguzi wengine hatutakiwi tufahamu kwa madai kwamba, tutatoa taarifa kwa wananchi na hatimaye kuwatia hofu”.

Awali, Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Aisha Kigoda alisema wananchi wanatakiwa kuwa makini na ugonjwa huo na kutoa taarifa mara wanapoona mtu mwenye dalili za ugonjwa huo.

Katika harakati za kukabiliana na ugonjwa huo, mwezi uliopita Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa alisema serikali imejizatiti kikamilifu kwa kuweka wataalamu wake mpakani, bandarini na viwanja vya ndege ambako huwapima watu wote wanaingia nchini kutoka nje.

Ugonjwa huo ambao dalili zake ni pamoja na homa ya ghafla, kuumwa kichwa, maumivu ya viungo, misuli na uchovu wa mwili umekuwa tishio duniani kote, lakini kwa nchi za Afrika wanaogundulika kuwa nao wengi wao ni wageni wanaotoka nchi za Ulaya.

Dalili nyingine za ugonjwa huo ni pamoja na kikohozi, mafua, maumivu yakoo, kichefuchefu, kusikia dalili za mwili kutetemeka na kukosa hamu ya kula chakula.

Wataalamu pia wanasema kwamba, wakati mwingine mgonjwa anaweza kuharisha na kutapika na kwamba wagonjwa wengine huzidiwa na kupata vichomi pamoja na kushindwa kupumua vizuri.

Wagonjwa wa kwanza wa homa ya mafua ya nguruwe waligundulika nchini Mexico Machi, mwaka huu na baadaye Marekani, kisha nchi za Ulaya. Afrika Msahariki na hasa Kenya waliwagunduka Juni wengi wao wakiwa wageni kutoka Ulaya.



Serikali yaunda tume kuchunguza ufisadi Tanesco

Mkurugenzi mkuu wa shirika la umeme Tanesco Dk Idris Rashid ambaye jana wabunge waliibua hoja ya ufisadi(Matumizi mabaya ya fedha za Serikali) unaoendelea kufanywa na shirika lake kinyume na sheria na taratibu za nchi.
Na Kizitto Noya, Dodoma

SIKU moja baada ya Mbunge wa Sumve (CCM), Richard Ndassa kuibua ufisadi wa Sh1.4 bilioni ndani ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), serikali imeunda tume kuchunguza tuhuma hizo.

Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja aliliambia gazeti hili jana kuwa tuhuma hizo ni nzito na hawezi kuacha zikapita bila kuzifanyia kazi.

“Mimi ndiyo kwanza nilizisikia bungeni na kimsingi nilipigwa butwaa, lakini sasa nimeanza kulishughulikia suala hilo kwa kuunda kamati ya uchunguzi,” alisema Ngeleja na kuongeza;

“Ninaamini kazi kubwa, lakini haitakuwa nzito sana kwani mheshimiwa mbunge ametusaidia kwa kutaja namba za nyumba zinazohusika”.

Ngeleja ambaye hakutaja idadi ya wajumbe wanaounda kamati hiyo wala muda watakaotumia kukamilisha kazi hiyo, alisema anaamini uchunguzi huo hautachukua muda mrefu.

Alisema kwa kuwa suala hilo limeibuliwa bungeni, ataweka matokeo ya uchunguzi huo hadharani ili wananchi wajue ukweli wake.

“Of Course (kwa ujumla) tuhuma hizo ni nzito, lakini siwezi kusema lolote zaidi ya kueleza kuwa ninazifanyia uchunguzi. Kazi imeanza leo (jana) na kwa sababu suala hilo limeibuliwa bungeni, tukimaliza kazi tutaijulisha jamii,” alisema Ngeleja.

Juzi jioni wakati akihitimisha mjadala wa wizara yake ya Nishati na Madini, Waziri Ngeleja aliliambia Bunge kuwa tuhuma hizo ni changamoto kwake na kwamba anajipanga kuishughulikia mara moja.

Aliliambia Bunge kuwa anathamini mchango wa mbunge huyo na kwamba isingekuwa rahisi kwake kufahamu jambo hilo kwa kuwa kinachoiunganisha wizara yake na Tanesco ni Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo.

Juzi mbunge wa Sumve Richard Ndassa aliibua ufisadi katika Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na kulieleza Bunge kuwa shirika hilo liko katika harakati ya kuiuza kwa Sh60 milioni nyumba namba 13 iliyoko Oysterbay jijini Dar es Salaam, mtaa wa Toure/Chaza line baada ya kuikarabati kwa Sh 600 milioni.

Sambamba na ufisadi huo, pia Shirika hilo linatuhumiwa kutumia Sh1.4 bilioni kukarabati nyumba sita za wakurugenzi kinyume na taratibu.

Ndasa alitoa tuhuma hizo alipokuwa akichangia bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini iliyowasilishwa Jumamosi iliyopita na waziri wake William Ngeleja.

Alisema fedha hizo ambazo ni sehemu ya mkopo wa Sh280 bilioni zilizokopwa benki kwa ajili ya kuendeleza miradi ya maendeleo ya Tanesco, imetumika bila ya idhini ya Bodi ya Wakurugenzi.

“Tanesco kuna matatizo makubwa yanayotokana na usimamizi mbovu na matumizi mabaya ya fedha. Shirika halina vipaumbele, linatumia vibaya fedha za umma,” alisema Ndasa na kuongeza:

”Mwaka 2007 shirika hilo lilikopa Sh280 bilioni kutoka benki mbalimbali kwa ajili ya miradi ya maendeleo, lakini badala ya kutekeleza vipaumbele, limeamua kukarabati nyumba za wakubwa kwa Sh 1.4 bilioni," alisema.



Ban ausihi ulimwengu ujirekibishe kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa

KM Ban Ki-moon, kwenye hotuba alioitoa Ulaanbaatar, mji mkuu wa Mongolia Ijumatatu ya leo, kuhusu "Marekibisho ya Kudhibiti Athari za Mabadiliko ya Hali ya Hewa Duniani" alieleza kwamba nchi zilizozungukwa na bara husumbuliwa sana na vizingiti vinavyokwamisha juhudi za kusukuma mbele maendeleo yao, hususan katika kipindi ambacho nchi hizi zisio na pwani huwa zinaathirika pia kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa,
kijumuisha pia taifa analolizuru la Mongolia, ambapo tatizo la kuenea kwa jangwa huko ni moja ya suala kuu linalozikaba nchi kama hizi kimaendeleo, hali ambayo hunyima umma fursa ya kupata riziki. Uharibifu wa maeneo ya malisho ya wanyama, au machungani, katika Mongolia, aliongeza kusema KM, huathiri sana uchumi wa taifa, na vile vile kuharibu mila na utamaduni wao. Watu wa Mongolia, alitanabahisha KM, ni miongoni mwa watu bilioni 2 ulimwenguni - sawa na thuluthi moja ya umma wa kimataifa - ambao hukabiliwa na hatari kuu ya kudhurika na kuenezwa kwa jangwa kwenye maeneo yao.

Ulinzi waimarishwa Nigeria Kaskazini

Mamlaka za nigeria zimeongeza ulinzi kwenye maeneo ya kaskazini mwa nchi hiyo kufuatiwa na mapigano yaliyoendelea kwa siku mbili na kuwaacha watu zaidi ya 100 wamekufa. Wanajeshi wameweka vizuizi barabarani katika

Mamlaka za nigeria zimeongeza ulinzi kwenye maeneo ya kaskazini mwa nchi hiyo kufuatiwa na mapigano yaliyoendelea kwa siku mbili na kuwacha watu zaidi ya 100 wamekufa.

Wanajeshi wameweka vizuizi barabarani katika maeneo yote yaliyoathiriwa na machafuko hayo ikiwemo miji ya Yobe, Kano, Borno na Plateau. Wanamgambo hao wa kiislam walivamia ofisi za polisi na ofisi za serikali.

Kuna taarifa zilizotolewa ya kuwa, kuna makundi ya vijana wenye silaha za mapanga na bunduki wakiiua polisi na raia ovyo.

Majeshi ya Nigeria na Polisi wameamuriwa kutumia kila njia kuhakikisha ulinzai wa nchi hiyo, iliripotiwa na mtangazaji wa shirika la habari la uingerza bi Caroline Duffield kutoka Nigeria.



Meli yaungua huko feri(Posta ya Zamani)


Meli ambayo inasemekana ni ya uvuvi iliyokuwa imeegeshwa pembezoni mwa bandari ya Dar es salaam (Feri posta ya zamani) imewaka moto na kunguu vibaya.

Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa meli hiyo ilikuwa imeegeshwa hapo kwa mda mrefu sana kwa sababu ya matengenezo yaliyokuwa yanendelea kwenye meli hiyo.

Dk. Mwakyembe ailipua Barrick


Mbunge wa Kyela (CCM), Dk. Harrison Mwakyembe, amependekeza kufungwa kwa mgodi wa dhahabu wa North Mara, unaomilikiwa na kampuni ya kimataifa ya uchimbaji madini ya Barrick Ltd kutokana na tuhuma za uchafuzi wa sumu katika maji ya mto Tigithe, ambapo watu kadhaa wamedaiwa kufa na wengine kuathirika.

Dk. Mwakyembe alisema hayo jana wakati akichangia hotuba ya makadirio ya matumizi ya fedha ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka 2009/10, iliyowasilishwa bungeni mwishoni mwa wiki na waziri wake, Wiliam Ngeleja.

“Pamoja na mapenzi mengi kwa wawekezaji, safari hii lazima tuchukue hatua dhidi ya mgodi wa North Mara, tufunge mgodi wa North Mara mpaka hatua itakapochukuliwa ya kurekebisha mfumo wake wa taka ya sumu,” alisema.

Alitaja hatua nyingine kuwa ni kuweka mpaka kati ya eneo la mgodi na makazi ya wananchi.

Dk. Mwakyembe alisema hatua kama hiyo pia ichukuliwe kwa

mgodi wa dhahabu wa Geita, uliopo mkoani Mwanza kwa kumwaga sumu kwa wananchi. Aliwataka wabunge wanaotoka maeneo hayo pamoja na wanasheria na wanaharakati kuwahamasisha wenzao kuifikisha mahakamani kampuni ya Barrick, kwa kuhatarisha maisha ya wakazi wanaozunguka migodi yao.

Alisema hatua hiyo itakuwa ni mwafaka kwao kwani haitatosha kupiga kelele majukwaani.

Baada ya kilio cha wakazi wa North Mara kuhusu uchafuzi wa maji yao, Bunge liliteua Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira chini ya Mwenyekiti wake, Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai (CCM), kwenda kufanya uchunguzi huo. Timu hiyo pia iliwahusisha wabunge wa Kamati ya Nishati na madini.

Ripoti hiyo imekwishakabidhiwa kwa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, lakini bado haijapangiwa ratiba ya kusomwa bungeni na wabunge kupata nafasi ya kuijadili.

Dk. Mwakyembe alisema kampuni ya Barrick inasifika duniani kwa uchafuzi wa mazingira na akaitaja Norway kuwa ni moja ya nchi ambayo iliifukuza kampuni hiyo nchini humo.

Katika hatua nyingine, Dk. Mwakyembe alitaka misamaha ya kodi kwa wawekezaji wa madini ifutwe na tena kwa makampuni yote, na akahoji ni kwanini wawekezaji kama hawa wanaogopwa.

Alitaka ununuzi wa mafuta nchini ufanywe kwa pamoja ili kuachana na utaratibu wa kuagiza mafuta kwa mtu mmoja mmoja, utaratibu ambao unachangia ongezeko la bei ya mafuta kwa wateja. Alisema utaratibu wa kuagiza mafuta kwa pamoja unatumika katika nchi za Malawi na Zambia na bei ya mafuta katika nchi hizo ni ndogo au inalingana na ile ya hapa.

Kama hiyo nayo haikutosha, Dk. Mwakyembe aliishukia Mamlaka ya Udhibiti wa Matumizi ya Nishati na Maji (Ewura), kwa kushindwa kuwadhibiti watu wanaochanganya mafuta ya taa na diezeli kwa manufaa yao ya kibiashara. Alisema Ewura inawafahamu wahusika hao na maeneo maarufu ya kuchakachua mafuta ambayo aliyataja kuwa ni kuanzia Kibaha hadi Chalinze, lakini mamlaka hiyo imeshindwa kuchukua hatua yoyote. Alisema anaipa Ewura muda wa miezi mitatu kufanya kazi na kama watashindwa atawasilisha bungeni hoja binafsi dhidi ya mamlaka hiyo. “Ewura tunawapa miezi mitatu, na mimi nitakuja na hoja hapa kuwataka Ewura wafanye kazi la sivyo waondoke, kama ni mshiko unawasumbua wafumbue macho,” alisema. Akizungumzia madini ya uranium yaliyogunduliwa nchini hivi karibuni, Dk. Mwakyembe alionyesha wasiwasi wake iwapo taifa limejiandaa vema kuchimba au hata katika kuweka mikabata mizuri ili uchimbaji utakapoanza uwanufaishe wananchi.

Alisema Tanzania sio nchi pekee katika Afrika kugundua kuwa ina madini hayo, kwani yameguliwa pia katika nchi nyingine 18 na akaitaka serikali kujifunza kutoka kwa nchi nyingine ambazo tayari zimeanza uchimbaji ili kuona namna gani madini hayo yanawanufaisha wananchi na mataifa yao kwa ujumla.

Alitaja baadhi ya nchi hizo kama Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Malawi na Uganda, ambazo Tanzania inaweza kujifunza na kisha kuamua namna bora zaidi ya kunufaika na madini hayo.

Alisema kama mambo hayo yatakuwa bado ni heri madini hayo yakaachwa kama ambavyo Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, alivyowahi kukataa kuchimbwa kwa madini kwa sababu taifa lilikuwa bado halijajiandaa. “Hizi ni habari njema, lakini natoa angalizo, ikiwa sisi viongozi tutaweka maslahi yetu mbele mbele na kuendekeza umimi katika uchimbaji wa madini hayo, tutazalisha ma Richmond na EPA wengine na kisha kusafishana kama tunavyofanya sasa,” alisema na kuongeza: “Ni heri madini hayo yaendelee kubaki ardhini.”

“Nyerere na Karume (Rais wa kwanza wa Zanzibar Aman Karume), walitaka madini yetu yasichimbwe, leo tunachimba sisi, lakini wanaofaidika ni nani. Tunashuhudia tunavyotoana macho sasa,” alisema.

Katika hatua nyingine, Dk. Mwakyembe aliishukuru serikali kwa uamuzi wa kuurudisha serikalini mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira, lakini akaomba wafanyakazi wa mgodi huo ambao hawajalipwa kwa miezi mingi sasa serikali iangalie namna ya kuwalipa.


Kiwanda cha kuchambulia pamba chateketea


Zaidi cha kilo milioni 1.6 za pamba safi zenye thamani ya Sh. Mililioni 726 zimeteketea kwa moto baada kiwanda cha kuchambua pamba cha Afrissian kilichopo katika kijiji cha Sanga wilayani Kwimba mkoani hapa kuteketea kwa moto.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Elias Kapinga, alisema kiwanda hicho kinamilikiwa na mfanyabiashara Ally Abush, mkazi wa mjini Shinyanga.

Alisema tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki, saa 11:00 alfajiri wakati maghala makubwa mawili na madogo yenye pamba safi kilo 1,650,000 yalipoteketea kwa moto ambao chanzo chake bado hakijajulikana.

Katika tukio hilo, wafanyakazi wawili wa kiwanda hicho, Andani ambaye ni meneja na Shinje Deus ambaye ni afisa ununuzi wa kiwanda walijeruhiwa baada ya kukatwa na mabati mapajani na usoni katika harakati za kujiokoa.


Wanaharakati wa kiislamu wauawa Nigeria


Takriban watu 150 wameuawa baada ya siku mbili za mashambulizi ya wanaharakati wa Kiislamu Kaskazini mwa Nigeria.

Mwandishi wa BBC amehesabu maiti 100 wengi wakiwa wanaharakati hao karibu na makao makuu ya polisi Maiduguri, jimbo la Borno , ambako mamia ya watu wamekuwa wakiyakimbia makaazi yao.

Walioshuhudia mashambulio hayo wameiambia BBC kwamba mapambano yaliendelea kwa muda wa saa kadhaa katika mji wa Potiskum, jimbo la Yobe na kituo cha polisi kiliteketezwa moto.

Mfumo wa elimu ya mataifa ya magharibi unapingwa

Baadhi ya wanaharakati hao ni wafuasi wa mhubiri Mohamed Yusuf ambae anaendesha kampeni dhidi ya mfumo wa elimu wa nchi za Magharibi.Bwana Yusuf anasema mfumo huo unakwenda kinyume na maadili ya kiislamu.

Wanaharakati wa kiislamu pia wameshambulia miji ya Wudil,kilometa 20 kutoka mji wa KANO-mji mkuu wa kaskazini mwa Nigeria. Amri ya kutotoka nje imetangazwa katika jimbo la Bauchi liliokumbwa na ghasia za siku ya Jumapili.

Wanaharakati waliokuwa wakisema Allahu Akbar kwa sauti kubwa walikishambulia kituo cha Polisi cha Potiskum saa nane alfajiri sambamba na mashambulio katika eneo la Maiduguri.

Mfumo wa sheria za kiislamu unatumika Kaskazini mwa Nigeria,ingawa hakuna historia ya mapambano yanayohusishwa na Al-Qaeda. Nigeria yenye wakaazi 150 millioni ina uwiano sawa kati ya waislamu na wakristo.Lakini kwa jumla jamii hizo mbili zinaishi kwa amani.

Kwa mujibu wa walioshuhudia, maiti zimesambaa mitaani Maiduguri baada ya kutolewa kutoka magari yao na kupigwa risasi .

Wafuasi wa Bwana Yusuf katika Bauchi wanajulikana kama Boko Haram, ikimaanisha elimu ya kimagharibi ni haramu.


Monday, July 27, 2009

Wanadiplomasia wa Marekani waongea na Mashariki ya Kati


Wanadiplomasia wa Marekani wapo katika mazungumzo huko Mashariki ya Kati ikiwa moja ya mipango ya nchi hiyo kujaribu kurejesha mazungumzo ya kuleta amani katika eneo hilo.

Wanadiplomasia wa Marekani wapo katika mazungumzo huko Mashariki ya Kati ikiwa moja ya mipango ya nchi hiyo kujaribu kurejesha mazungumzo ya kuleta amani katika eneo hilo.

Waziri wa ulinzi wa Marekani bwana Robert Gates amepanga kukutana na waziri wa ulinzi wa Israel bwana Ehud Barak halafu atakutana pia na waziri mkuu wa Israel bwana Benjamin Netanyahu

Mwanadiplomasia wa Marekani bwana George Mitchell aliwasili Egypt akitokea kwenye maongezi Syria na Israel atakutana na rais Hosni Mubarak.

Mazungumzo hayo ya amani ya Israel - Parestina yakiwa yanaendelea na vitisho vinavyotolewa na Iran, navyo vimewekwa kwenye ajenda ya maongezi hayo.

Huko Tel Aviv jumapili, bwana Mitchell aliwahakikishia wawakilishi wa Israel juuu ya msimamo usiotetereka wa serikali ya Washington kuhusu ulinzi wa taifa hilo.


Waziri wa usalama wa Iran atimuliwa

Rais wa Iran bwana Mahmoud Ahmadinejad amemuachisha kazi waziri wake wa ulinzi siku mabayo ilimbidi aghailishe uteuzi wa makamu wa Rais. Sababu ya kumuachisha wadhifa huo waziri huyo

bwana Gholam Hossein Mohseni Ejeie hazijatolewa. Wakati huohuo waziri wa utamaduni amejiuzuru, akisema kuwa serikalini kuna matatizo.

Rais huyo anatarajiwa kuitangaza baraza lake la mawaziri baada ya kula kiapo kwa mara ya pili ndani ya siku 10, baada ya ushindi wake wa utata wa kiti cha urais.

Pamoja na matatizo hayo, ofice ya rais huyo imekanusha taarifa za kufukuzwa kwa mawaziri wengine watatu.





Marekani na Amani Mashariki ya Kati


Marekani imeitaka Syria kutoa ushirikiano wa dhati katika juhudi za kufikia makubaliano ya amani katika ukanda wa Mashariki ya Kati.

Akizungumza baada ya mazungumzo mjini Damascus nchini Syria, mjumbe maalum wa Rais Obama kuhusu Mashariki ya Kati George Mitchell amesema mazungumzo yake na Rais wa Syria yamekuwa ya wazi na matumaini.

Bwana Mitchel amesema mpango wa kuazishwa tena kwa mazungumzo ya amani kati ya Syria na Israeli unakaribia kufikiwa hivi karibuni.

Anatarajiwa kuelekea Israeli katika juhudi za kuanzisha mazungumzo kati ya Israeli na Palestina.

Ziara ya Bwana Mr Mitchell nchini Syria ni ya pili toka mwezi Juni katika juhudi mpya za Marekani kuhimiza amani Mashariki ya Kati toka Rais Obama aingie madarakani mwanzoni mwa mwaka huu.

Ziara hii inafuatia msururu wa ziara kadhaa zilizofanywa na maafisa wa utawala wa Rais Obama nchini Israeli wiki hii, katika kipindi ambacho mahusiano kati ya Marekani na Israeli yakiwa katika mvutano usio wa kawaida.

'Juhudi za kihistoria'

Bwana Mitchell amesema amemwambia rais wa Syria Bashar Assad kwamba Rais Obama amedhamiria kusaidia makubaliano ya kweli ya amani kati ya waarabu na Israeli.

Kwa kawaida katika mahusiano ya kirafiki kati ya pande mbili ni vigumu kukubaliana kila jambo.

''Lengo letu ni kuleta katika eneo hili na watu wake wote fursa ya kuishi kwa amani na heshima. Ili kufanikiwa tutahitaji waarabu pamoja na waisraeli kushirikiana nasi ili kuleta suluhu kamili.
Tunakaribisha ushiriano wa serikali ya jamhuri ya kiarabu ya Syria katika juhudi hii ya kihistoria''. Alisema Bwana Mitchell.

Nao maafisa wa Syria wamesema wametiwa moyo na kile mmjawao amekielezea kama msimamo mpya wa marekani wa kukubali kusikiliza mambo, tangu Rais Obama aingie madarakani mwanzoni mwa mwaka huu.

Damascus ni kiungo muhimu katika ukanda huu kutokana msimamo wake wa kuuunga mkono kundi la wapiganaji la Hamas, kusaidia Hezbollah nchini Lebanon, na pia kutokana na mahusiano yake ya karibu na Iran.


WAGONJWA TARAFA YA KATERERO WALALA NA MAITI WODINI!!

Na Anna Nkinda - Maelezo 27-07-2009
Katoro Wagonjwa wa kijiji cha Katoro kata ya Katoro Tarafa ya Katerero wilaya ya Bukoba vijijini wanaolazwa katika kituo cha afya Katoro wanakabiliwa na tatizo la kulala na maiti wodini kutokana na kituo hicho kutokuwa na chumba cha kuhifadhia maiti.
Hayo yamesemwa jana na daktari Mfawidhi wa kituo hicho Augustine Mnyamukama wakati akisoma risara ya watumishi kwa mke wa Rais Mama Salma Kikwete aliyefika kituoni hapo kwa ajili ya kutoa vitanda vya kujifungulia viwili, vitanda vya kawaida vitano na mashuka kumi. "Kama mgonjwa akifariki katika kituo chetu hakuna mahali pa kuhifadhia maiti jambo ambalo linawafanya wagonjwa wa wodi husika kulala na maiti hadi ndugu wa marehemu watakapokuja kuichukua maiti na kwenda kuizika", alisema.
Dk. Mnyamukama aliyataja matatizo mengine yanayoikabili kituo hicho kuwa ni upungufu wa watumishi, upungufu wa madawa muhimu pamoja na vifaa, vitanda vya kuzalishia na vya kawaida, hakuna wodi maalum ya akina mama wajawazito na wanaume, kutokuwepo kwa huduma ya upasuaji wa dharula , nyumba za watumishi, umeme na maji. Aliendelea kusema kuwa pamoja na matatizo hayo jitihada za pamoja zinafanyika kati ya wananchi na Serikali ili kuweza kutatua matatizo hayo. "Hivi sasa tumefanikiwa kupata gari la kusafirisha wagonjwa wa dharula hali iliyosababisha kupungua kwa vifo wa watoto na kina mama wajawazito, tunatoa huduma ya Ugonjwa wa UKIMWI pia Halmashauri ya wilaya ya Bukoba kwa kushirikiana na wafadhili (JRF) wamewezesha kukarabatiwa kwa wodi ya watoto", alisema. Aliyataja magonjwa yanayowasumbua wananchi wa eneo hilo kuwa ni maralia, magonjwa ya nayoshambulia mfumo wa hewa, kuharisha, minyoo, upungufu wa damu, vichomi na magonjwa yanayosababishwa na virusi vinavyosababisha Upungufu wa Kinga Mwilini.
Akikabidhi vifaa hivyo Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) aliwataka wananchi wa eneo hilo kuvitunza vifaa hivyo ili viweze kutumika kwa muda mrefu kwa vizazi vijavyo. "Katika maeneo mengine wananchi wamekuwa wakiharibu na hata kuiba vifaa mbalimbali vinavyotolewa na wafadhili jambo ambalo limekuwa likikatisha tamaa na kurudisha nyuma maendeleo ya nchi", alisema.
Kituo hicho kipo umbali wa kilomita 58 kutoka Hospitali ya mkoa kilijengwa mwaka 1947 kikiwa zahanati na ilipofika mwaka 1974 kilipandishwa hadhi na kuwa kituo cha Afya kinahudumia zaidi ya wakazi 13,574 pamoja na kuhudumia zahanati za Kishogo, Butainamwa, Kaibanja, Ruhunga, Kihumulo na Kyamulaile.
Kwa upande wa tiba kituo hicho kinatoa huduma ya wagonjwa wanaotibiwa nyumbani na kurudi (OPD), kutibu wagonjwa kwa wastaini 90 kwa siku na kulaza wagonjwa wa wastani kumi na tisa kwa siku. Pia kituo kinatoa huduma za kinga kwa mama na mtoto, uzazi wa mpango, elimu ya afya kwa jamii, huduma ya mkoba, kuzuia maambukizi ya Virusi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na upimaji wa virusi kwa hiari.
Mama Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku tatu katika mkoa wa Kagera yenye lengo la kuchangia juhudi za kupunguza vifo vya kinamama vinavyotokana na uzazi kwa kutoa vifaa vya huduma ya afya ya uzazi, hususan katika wodi za wazazi. Kuhamasisha juhudi za maendeleo kwa wanawake kupitia vikundi vya SACCOS na benki za vijijini- VICOBA. Kuhamasisha juhudi za kupunguza matukio ya mimba na utoro mashuleni, kuhamasisha vikundi vya SACCOS na benki za vijijini- VICOBA na kuhamasisha juhudi za kupunguza matukio ya mimba na utoro mashuleni.


TRA sasa yafuatilia matumizi ya taasisi za kidini na NGOs

Baada ya serikali kusitisha uamuzi wake wa kuzifutia taasisi za dini na mashirika yasiyo ya kiserikali (NGOs) misamaha ya kodi, sasa imeagiza mashirika hayo kufuatiliwa.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeagizwa kutafiti misamaha ya kodi inayoitoa kwa madhehebu ya dini na NGOs, kwa lengo kudhibiti matumizi mabaya ya misaada hiyo.

Agizo hilo limetolewa na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mukulo, mwishoni mwa wiki mjini hapa wakati akizungumza na wafanyakazi wa TRA mkoani hapa kwenye ukumbi wa mikutano wa jengo la mamlaka hiyo wakati wa ziara ya kikazi ya siku mbili.

Mkulo alisema kuwa hatua hiyo itasaidia kubaini waombaji wanaotumia misamaha hiyo kujinufaisha wao binafsi, hivyo kuikosesha serikali mapato kwa ajili ya kuwaletea wananchi maendeleo.

Waziri huyo alisema uzoefu unaonyesha kuna baadhi ya watu wamekuwa wakitumia vibaya misamaha ya kodi kwa kuingiza vifaa mbalimbali, na mali zingine bila kulipa kodi, hivyo kuikosesha serikali mapato.

Akiwasilisha bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2009/10 bungeni Juni 11, mwaka huu, Mkulo alitangaza uamuzi wa serikali wa kufuta misamaha ya Kodi la Ongezeko la Thamani (VAT) kwa mashirika ya dini na NGOs kwa maelezo kuwa baadhi ya taasisi hizo zimekuwa zikiitumia vibaya misamaha hiyo.

Uamuzi huo wa serikali ulipingwa vikali na viongozi wa taasisi za dini, ambao walisema utawazuia kama wadau wa maendeleo kutoa misaada kwa jamii hususan huduma za afya, elimu na miundombinu.

Shinikizo hilo liliilazimisha serikali kusitisha uamuzi huo baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kukutana na viongozi wa taasisi za dini mjini Dodoma na kukubaliana kuunda kamati ya pamoja ya kufuatilia na kuhakikisha kuwa misamaha hiyo haitumiki vibaya.

Mbali na uamuzi huo kupingwa na taasisi za dini, lakini pia wabunge kadhaa waliochangia hotuba ya bajeti waliishauri serikali kusitisha hatua hiyo kwa hoja kwamba inasababisha kuzorota kwa huduma za jamii kutokana na taasisi hizo kutoa mchango mkubwa.

Aidha, Waziri Mkulo ameagiza kubana mianya yote inayopitisha bidhaa mbalimbali ili kuiongezea serikali mapato.

Meneja wa TRA Mkoa wa Singida, Jumbe Samson, alisema katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2008/2009, wamekusanya mapato ya zaidi ya Sh. bilioni 1.4.

Kwa mujibu wa Samson, kiasi hicho ni sawa na asilimia 79.4 ya lengo lililokusudiwa la kukusanya Sh. 1,797,700,000 walizopangiwa na Makao Makuu ya TRA.