
Mahakama ya juu nchini India imeitaka serikali kutafakari hatua ya kuhalalisha biashara ya ukahaba ikiwa haiwezi kuikomesha.
Mahakama hiyo imesema ikiwa serikali itahalalisha biashara hiyo, makahaba huenda wakarebisha tabia yao huku biashara ya ulanguzi wa wanawake ikizuiwa.
Matamshi ya mahakama yamejiri wakati ikisikiliza kesi kuhusu biashara ya ulanguzi wa watoto iliyofikishwa mahakamani na shirika lisilo la kiserikali.
Ukahaba umepigwa marufuku nchini India lakini biashara hiyo imenawiri katika baadhi ya miji. Kuna takriban makahaba milioni mbili nchini India.
0 comments:
Post a Comment