Shirika la kimataifa linaloshughulikia maslahi ya wahamiaji, IOM linasema mamia ya wahamiaji kutoka Afrika na Asia wamekwama nchini Iraq.
Wahamiaji hao wanasumbuka kwani hawana fedha za kuwasaidia kuondoka nchini humo.
Msemaji wa shirika hilo Jemini Pandya amesema wanatafuta dola milioni mbili unusu kuwasaidia wahamiaji 700 wanaondelea kuhangaika nchini Iraq.
Amesema kwa miaka sita shirika lake limekuwa likiwasaidia wahamiaji 7,000 lakini ni 32 pekee walioweza kuokolewa mwaka huu.
Ameongeza wahamiaji wengi walihadaiwa kusaini mikataba ya kazi zisiszo za kweli nchini Iraq.
Wengi hupokonywa hati zao za kusafiria na hufanya kazi katika mazingira mabovu.
0 comments:
Post a Comment