TANGAZA BIASHARA YAKO HAPA KWA BEI NAFUU / ADVERTISE YOUR BUSINESS HERE AT CHEAP RATES | CONTACT ME: kilinyepesi@gmail.com

 photo DTB_zps7bd2662d.jpg

 photo fl_zps09337f7a.jpg


Habari Mpya:
Wednesday, December 16, 2009

Vituo 13 vya mafuta vyakamatwa Dar

9:12 PM

Wakala wa Vipimo na Mizani Tanzania, wamekamata mashine 13 za kuuza mafuta ya petroli Dar es Salaam zilizogundulika kufanyiwa udanganyifu, ili kuwaibia wateja.

Operesheni iliyoendeshwa jana, katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, ilibaini mashine hizo katika vituo vitatu, na kuvipiga marufuku kuendesha biashara hiyo.

Kwa mujibu wa mkuu wa operesheni hiyo Wilbroad Kimaro, msako huo umelenga kuhakikisha kuwa watu wanapata huduma zinazolingana na fedha wanayotoa.

Hivi karibuni Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji, Ewura, Haruna Masebu, alibainisha kuwa zaidi ya asilimia 70 ya vituo vyote 900 nchini vinajihusisha na udanganyifu katika biashara hiyo.

0 comments:

Post a Comment

 
BONYA HAPA