
KIKWETE ATIA DOA BAADA YA KUSHINDWA KUTOKEA UKUMBINI, DK SHEIN, MWINYI, KARUME, NAHODHA, DK SALIM, WARIOBA, WATINGA
Ramadhan Semtawa
EDWARD Lowassa, ambaye alijiuzulu uwaziri mkuu kutokana na kashfa ya mkataba wa kifisadi kati ya kampuni ya Richmond Development (LLC) na Tanesco, juzi alitikisa Jiji la Dar es Salaam baada ya sherehe ya kumuaga bintiye anayeitwa Dk Anna kuvuta vigogo wengi akiwemo makamu wa rais, Dk Ali Mohamed Shein na rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi.
Sherehe hiyo kubwa iliyofanyika Desemba 8 mwaka huu kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, ilianza majira ya 12:30 jioni na kumalizika saa 7:30 usiku, lakini Rais Jakaya Kikwete alishindwa kuhudhuria na kutoa udhuru dakika za mwisho.
Wingi wa vigogo hao waliohudhuria sherehe hiyo unaweza kuzidi hata idadi ya vigogo waliohudhuria sherehe za miaka 48 ya uhuru wa Tanganyika zilizofanyika kesho yake kwenye Uwanja wa Uhuru.
Wakati mawaziri wa zamani na vigogo wengine hawakuhudhuria sherehe za uhuru, hali ilikuwa tofauti kwenye sherehe ya kumuaga binti Lowassa ambazo zilihudhuriwa na vigogo wengi wa CCM na serikali, ukiacha Rais Kikwete, Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Spika wa Bunge Samuel Sitta na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe.hapa zaidi
0 comments:
Post a Comment