
Viongozi wa Muungano wa ulaya wanakabiliwa na kibarua kigumu kuhusu kiwango cha pesa watakachotoa kwa hazina ya kimataifa kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya anga.
Viongozi wa Uingereza na Ufaransa, waziri mkuu Gordon Brown na rais Nicolas Sarkozy wanaokutana Brusselas, wamesema nchi zao zitatoa kima cha dola bilioni moja nukta tano kutumika kwa miaka mitatu.
Viongozi hao wamesema ni sharti mkutano wa Copenhagen uidhinishe kile wametaja kuwa hazina ya ufunguzi kusaida nchi maskini kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali ya anga.
Wamesema mkataba wowote utakoafikiwa sharti utimizwe katika muda wa miezi sita na sharti uruhusu kuongezwa mdaada hadi mwaka 2020.
0 comments:
Post a Comment