
Dawa maalum ya kupaka ambayo ilikusudiwa kuzuia maambukizi ya ukimwi haijafanikiwa, baada ya majaribio makubwa ya kimataifa kuwahi kufanyika.
Baraza la utafiti wa matibabu nchini Uingereza ambalo liligharamia majaribio hayo katika nchi za Afrika, limeelezea matokeo yake kuwa ya kuvunja moyo baada ya kuwepo na matumaini makubwa na vile vile kuwekeza fedha nyingi katika mradi huo.
Zaidi ya wanawake elfu tisa katika nchi nne za Kusini mwa jangwa la Sahara walishiriki katika majaribio hayo.
Wanawake hao walipewa krimu ya kupaka kwenye sehemu zao za siri iitwayo PRO 2000 ambayo ilitakiwa kupakwa kabla ya kujamiiana.
Barani Afrika zaidi ya asilimia 60 ya walioambukizwa virusi vya HIV na Ukimwi ni wanawake na wengi wao waliambukizwa kutokana na wapenzi wao waasharati.
Majaribio mengine yanaendelea kufanywa lakini Dkt. Sheena McCormack wa baraza la utafiti wa matibabu la Uingereza anasema matokeo "yanavunja moy
0 comments:
Post a Comment