Rais wa Iran bwana Mahmoud Ahmadinejad amemuachisha kazi waziri wake wa ulinzi siku mabayo ilimbidi aghailishe uteuzi wa makamu wa Rais. Sababu ya kumuachisha wadhifa huo waziri huyo bwana Gholam Hossein Mohseni Ejeie hazijatolewa. Wakati huohuo waziri wa utamaduni amejiuzuru, akisema kuwa serikalini kuna matatizo.
Rais huyo anatarajiwa kuitangaza baraza lake la mawaziri baada ya kula kiapo kwa mara ya pili ndani ya siku 10, baada ya ushindi wake wa utata wa kiti cha urais.
Pamoja na matatizo hayo, ofice ya rais huyo imekanusha taarifa za kufukuzwa kwa mawaziri wengine watatu.
| |
0 comments:
Post a Comment