
Wanadiplomasia wa Marekani wapo katika mazungumzo huko Mashariki ya Kati ikiwa moja ya mipango ya nchi hiyo kujaribu kurejesha mazungumzo ya kuleta amani katika eneo hilo.
Wanadiplomasia wa Marekani wapo katika mazungumzo huko Mashariki ya Kati ikiwa moja ya mipango ya nchi hiyo kujaribu kurejesha mazungumzo ya kuleta amani katika eneo hilo.
Waziri wa ulinzi wa Marekani bwana Robert Gates amepanga kukutana na waziri wa ulinzi wa Israel bwana Ehud Barak halafu atakutana pia na waziri mkuu wa Israel bwana Benjamin Netanyahu
Mwanadiplomasia wa Marekani bwana George Mitchell aliwasili Egypt akitokea kwenye maongezi Syria na Israel atakutana na rais Hosni Mubarak.
Mazungumzo hayo ya amani ya Israel - Parestina yakiwa yanaendelea na vitisho vinavyotolewa na Iran, navyo vimewekwa kwenye ajenda ya maongezi hayo.
Huko Tel Aviv jumapili, bwana Mitchell aliwahakikishia wawakilishi wa Israel juuu ya msimamo usiotetereka wa serikali ya Washington kuhusu ulinzi wa taifa hilo.
0 comments:
Post a Comment