
Vikosi vya Nigeria vimeushambulia msikiti mmoja ambako wapiganaji wa kundi moja la Kiislamu linalolaumiwa kwa kuzusha ghasia limekuwa likijificha.
Taarifa zinaelezea kwamba wapiganaji wengi wameuawa katika mapigano hayo, ambayo yamefanyika siku ya tatu tangu ghasia kuzuka katika mji wa kaskazini wa Maiduguri.
Wengi ya wapiganaji hao sasa wametoroka, huku wakivishambulia vituo kadha vya polisi.
Kundi hilo la wapiganaji la Kiislamu, linalofahamika kama Boko Haram, linataka kuipindua serikali, na kuanzisha mfumo wa sharia za Kiislamu katika kuiongoza nchi.
Vikosi viliushambulia msikiti huo, baada ya wanajeshi 1,000 zaidi kupelekwa katika mji huo.
Kamanda wa wanajeshi wa nchi kavu, Meja Jenerali Saleh Maina, aliliambia shirika la habari la Associated Press kwamba naibu wa kiongozi wa kundi hilo, aliuawa katika mapigano hayo, usiku wa Jumatano.
0 comments:
Post a Comment